2014-08-15 11:29:00

Maombi kwa ajili ya Wakristo Wateswa wa Ulaya iliyowekwa pembezoni


Ijumaa hii Agosti 15, ambamo Kanisa limeadhimisha Siku Kuu kubwa ya Bikira Maria kupalizwa mbinguni, nchini Italia, Kanisa limetolea sala zake kwa nia ya kuombea Wakristo wote wanaoishi katika hali ngumu za mateso kwa ajili ya imani yao.
Baraza la Maaskofu la Italia( CEI) lilitangaza nia hii, kama sehemu ya kutoa jibu, lenye kukubaliana na wito wa Papa Francisko, katika kukabiliana mateso kwa Wakristo leo hii , kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza. Na hivyo, CEI ilitoa mwaliko kwa jumuiya zote za Kanisa kujiunga katika sala kama ishara halisi ya ushiriki na wote wanaoteswa na ukandamizaji mkali. Ujumbe wa Baraza la Maaskofu la Italia CEI, unasema, "Hatuwezi kukaa kimya hasa mbele ya" Ulaya ya yetu, inayo raruliwa na kubadilishwa, na kuwa na upofu na ububu mbele ya mateso ambayo leo, waathirika ni amia ya maelfu ya Wakristo. haya yameelezwa na Katibu Mkuu wa CEI, Mons. Nunzio Galantino, ameeleza wakati wa mahojiano na Marco Guerra, wa Redio Vatican.

Na kwamba kutokana na hali hizi za kusikitisha na kutisha wanazoziishi Wakristo ktiak baadhi ya maeneo, kuna haja kupaza sauti na kusema sasa basi yatosha, si tu barani Ulaya, lakini pia katika mataifa mengine, kama ilivyo huko Yazidis Iraq, Syria, Nigeria na kwingineko. Ni kuwa na mwamko zaidi katika kuweka wazi zaidi maamuzi juu ya suala hili, kutokana na umuhimu wake wa kutotumia nguvu katika kuwaondoa katika mateso ndugu zetu hawa, kaka na dada zetu wanaoteseka na hasa wale wanaoendelea kuvumilia yote na kudumu na imani yao.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mons, Galantino kwa ujumla, Kanisa nchini Italia limeonyesha mshikamano mzuri na Wakristo wateswa hasa wanaoteseka Iraki, ingawa jawabu la suala hili si sawa kwa sehemu zote , kuna maeneo mengine ambayo kweli yanahitaji msaada wa kihali hasa wale waliokimbia na sasa wanaishi katika kambi, au katika majengo ya taasisi wanakoona ni salama zaidi kwa maisha yao kama ilivyo Samir, katika Parokia ya Mtakatifu Joseph, ambao wameomba msaada moja kwa mojaNa akizungumzia juhudi za kusitisha ukatili dhidi ya makundi madogomadogo ya kidini anasema, kwa maoni yake, awali ya yote, ni kupata taarifa za yote yanayoendelea, kujua watu wote wanafanya nini na kwa nini chuki hii ya mauaji na mateso kwa watu wasiokuwa na hatia. Na hivyo Wakatoliki wa Italia , tangu siku ya leo Agosti 15, kwa namna mbalimbali wanatafuta kupata ufahamu hata zaidi juu ya madhulumu haya kwa Wakristo. Na katika uwezo wake , CEI tayari imetenga fedha, kwa ajili ya kushughulikia tatizo hili. Maaskofu wamepania kweli kusitisha chuki hii ya mauaji, hivyo wanaitahadharisha dunia nzima, itoe angalisho makini si tu katika nchi za Magharibi, lakini na kwingineko dhidi ya janga hili.
Na Kardinali Bagnasco, Rais wa CEI, anasema, sala ni tendo la kwanza muhimu linalowaunganisha na waamini wateswa na wahitaji wote kwenye parokia na vigango vyote vilipo. Na hivyo kwa pamoja Kanisa nchini Italia lilitangaza tarehe 15 Agosti, iwe siku maalum ya kuugana kiroho na kihali na watu wote wanaoteseka kwa sababu ya imani yao. Ameeleza haya na kutaja jinsi Baba Mtakatifu Francisko anavyoumizwa na taarifa za madhulumu haya, na kulazimika kukemea na kuitaka jumuiya ya kimataifa iingilie kati, kusitisha dhuluma hizi.







All the contents on this site are copyrighted ©.