Salam za rambi rambi kutokana na ajali ya ndege Iran
Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambi rambi kwa Askofu mkuu Ignazio Bedin,
Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Iran kufuatia ajali ya ndege ya abiria iliyosababisha
vifo vya watu zaidi ya arobaini, Jumapili tarehe 10 Agosti 2014.
Baba Mtakatifu
anasema amepokea taarifa ya ajali hii kwa masikitiko makubwa na kwamba, anamwomba,
amfikishie salam zake za rambi rambi kwa ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba
huu.
Katika ujumbe huu ambao umetiwa sahihi na Kardinali Pietro Parolin, Katibu
mkuu wa Vatican, Baba Mtakatifu anapenda kuwafariji na kuwapatia baraka na amani wote
wanaoombeleza msiba huu mzito.