Tarehe 10 Agosti, 2014 ni siku ya kuombea amani, umoja na mshikamano wa kitaifa Korea!
Baraza la Makanisa Ulimwenguni linayaalika Makanisa wanachama kushikamana kwa njia
ya sala, ili kuombea, amani, umoja na mshikamano kati ya Korea ya Kusini na Korea
ya Kaskazini, Jumapili tarehe 10 Agosti 2014.
Huu ni mwendelezo wa Mapokeo
kwa ajili ya kuomba umoja na mshikamano wa kitaifa kila Jumapili ya Mwaka kabla ya
tarehe 15 Agosti, Siku ambayo Korea ya Kusini na Korea ya Kaskazini zinasherehekea
Siku kuu ya Ukombozi.
Itakumbukwa kwamba, Korea ilijipatia uhuru wake kutoka
kwa Mjapani kunako tarehe 15 Agosti 1945, lakini hii pia ndiyo siku iliyoisambaratisha
Korea na kujikuta imegawanyika sehemu kuu mbili, yaani Korea ya Kaskazini na Korea
ya Kusini. Kusali kwa ajili ya kuombea amani na mshikamano wa kitaifa ni kielelezo
cha hali ya juu kinachoweza kuoneshwa na Baraza la Makanisa Ulimwenguni.
Huu
ni mwendelezo wa maazimio ya mkutano mkuu wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni uliofanyika
mjini Busan, Korea ya Kusini, ili kuendelea kuunga mkono hija ya maisha ya kiroho
inayofanywa na Korea hizi mbili katika mchakato wa ujenzi wa misingi ya haki, amani
na maisha.