Mwenyezi Mungu, watie shime wananchi wa Iraq ambao wanakosa mahitaji yao msingi kwa
sasa!
Mashambulizi yaliyokuwa yanafanywa na Jeshi la Jihadi, Kaskazini mwa Iraq yamesababisha
maafa makubwa kwa watu na mali zao, kiasi cha kuwafanya Wakristo wengi kuyakimbia
makazi yao. Hali inazidi kuwa ngumu kwa wakati huu, ambapo Marekani imeamua kupambana
na Jeshi la Jihadi, kwa kujielekeza katika ngome za majeshi haya, hasa katika eneo
la Makhmur.
Taarifa za kijeshi zinasema kwamba, Marekani itaendelea kushambulia
maeneo yote yanayokaliwa kwa mabavu na Jeshi la Jihadi, kutokana na mwelekeo huu hali
imekuwa tata zaidi huko Iraq.
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake
wa tatu, alioutoa Ijumaa usiku tarehe 8 Agosti 2014 anamwomba Mwenyezi Mungu, aweze
kuwatia shime wananchi wa Iraq ambao wanateseka kwa wakati huu kwa kukosa mahitaji
yao msingi.