2014-08-08 11:59:49

Ujumbe kwa Siku ya Wenyeji Kimataifa kwa Mwaka 2014


Jumuiya ya Kimataifa tarehe 9 Agosti 2014 inasherehekea Siku ya Wenyeji Kimataifa kwa kuangalia kwa namna ya pekee haki msingi za binadamu kama njia ya kujenga jamii shirikishi. Sheria nyingi za kitaifa na kimataifa zinachota utajiri wake kutoka katika Tamko la Haki Msingi za Binadamu lililotolewa na Umoja wa Mataifa.

Lakini, Jumuiya ya Kimataifa bado ina safari ndefu inayopaswa kutekelezwa kwa kusimama kidete kupambana kufa na kupona na umaskini unaowaandama wenyeji wengi, kiasi hata cha kubaguliwa na kutengwa katika maamuzi ya kisiasa na kiuchumi. Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya wenyeji kimataifa kwa mwaka huu ni "Tuondoe kinzani: tutekeleze haki msingi za wenyeji".

Watu hawana budi kujifunga kibwebwe katika kupambana na ubaguzi, kwa kujenga na kudumisha utamaduni wa kuheshimiana, kulinda na kuendeleza urithi wa kimataduni unaopatikana miongoni mwa watu.







All the contents on this site are copyrighted ©.