2014-08-08 10:40:48

Shikamaneni na watu waliotikiswa kwa ugonjnwa wa Ebola!


Baraza la Makanisa Ulimwenguni limeguswa sana na hali ya hatari iliyojitokeza Afrika Magharibi kutokana na kuenea kwa ugonjwa wa Ebola ambao kwa sasa umekuwa ni tishio kwa afya ya umma na kwamba, una madhara makubwa kwa wananchi wanaoishi Afrika Magharibi kwa sasa.

Ugonjwa wa Ebola ni hatari kwani haubugui wala hauchagui, linasema Baraza la Makanisa Ulimwenguni katika taarifa yake. Baraza hili linazihimiza Serikali, Makampuni binafsi na wataalam wa wafya kushikamana kwa hali na mali katika kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi.

Taasisi za afya zinazomilikiwa na kuendeshwa na Makanisa katika maeneo yaliyokumbwa na ugonjwa wa Ebola, yawe mstari wa mbele kuwasaidia waathirika kwa kutambua unyeti wa ugonjwa wenyewe! Baraza la Makanisa Ulimwenguni linaendelea kuwakumbuka wote waliotikiswa kwa ugonjwa wa Ebola katika sala na maombi yake!







All the contents on this site are copyrighted ©.