Kitabu cha Tatu chenye Mahubiri ya Papa Francisko kimechapishwa
Taasisi ya Uchapisha vitabu ya Libreria Editrice Vatican “LEV” mapema Ijumaa hii
08 Agosti 2014, ilichapisha toleo la tatu la kitabu chenye mahubiri ya Papa Francisko.
Kitabu hicho kinatoa mafundisho ya Papa Francisko juu ya masomo na Injili, zilizo
somwa kila siku, wakati wa Maadhimisho ya Ibada za Misa Takatifu nyakati za mapema
asubuhi, katika kanisa dogo la Mtakatifu Marta “Domus Sanctae Marthae” la ndani
ya Vatican, katika kipindi cha tangu Februari 3 hadi Juni 30, 2014.
Kitabu
kina jumla ya mahubiri 64 ikiwa ni pamoja na mahubiri mengine aliyo yatoa siku
za maadhimisho ya Ibada za Kipapa na pia mahubiri aliyo yatoa wakati akiongoza Ibada
kwa ajili ya Wabunge wa Italia, asubuhi ya tarehe 27 Machi katika Kanisa Kuu la
Mtakatifu Petro Vatican. Kati ya mada alizozungumzia Papa Francisko ni Ubaba wa Mungu
, siri ya kifo, upinzani na majaribu, msimamo wa Ukristo, mateso na mauaji, huruma,
wito kwa unyenyekevu, maombi na nguvu ya ushahidi
Maandishi haya ni mkusanyiko
wa mahubiri yaliyo chapishwa kila siku katika gazeti la L'Osservatore Romano kama
sehemu ya mfululizo wa Mafundisho ya Papa Franciskco, ambayo tayari yana majina mengine:
Tafadhali ombeni kwa ajili yangu, msiachie tumaini lenu kuibiwa na mengine, furaha
kuinjilisha, ni vizuri kuwa hapa, kutembea kwenye njia ya amani, Yesu daima anavuta
subira kwa ajili yetu, Chemichemi za imani, na tujifunue kwa mwanga wa Bwana.