2014-08-08 12:46:58

Kitabu cha Tatu chenye Mahubiri ya Papa Francisko kimechapishwa


Taasisi ya Uchapisha vitabu ya Libreria Editrice Vatican “LEV” mapema Ijumaa hii 08 Agosti 2014, ilichapisha toleo la tatu la kitabu chenye mahubiri ya Papa Francisko. Kitabu hicho kinatoa mafundisho ya Papa Francisko juu ya masomo na Injili, zilizo somwa kila siku, wakati wa Maadhimisho ya Ibada za Misa Takatifu nyakati za mapema asubuhi, katika kanisa dogo la Mtakatifu Marta “Domus Sanctae Marthae” la ndani ya Vatican, katika kipindi cha tangu Februari 3 hadi Juni 30, 2014.

Kitabu kina jumla ya mahubiri 64 ikiwa ni pamoja na mahubiri mengine aliyo yatoa siku za maadhimisho ya Ibada za Kipapa na pia mahubiri aliyo yatoa wakati akiongoza Ibada kwa ajili ya Wabunge wa Italia, asubuhi ya tarehe 27 Machi katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican. Kati ya mada alizozungumzia Papa Francisko ni Ubaba wa Mungu , siri ya kifo, upinzani na majaribu, msimamo wa Ukristo, mateso na mauaji, huruma, wito kwa unyenyekevu, maombi na nguvu ya ushahidi

Maandishi haya ni mkusanyiko wa mahubiri yaliyo chapishwa kila siku katika gazeti la L'Osservatore Romano kama sehemu ya mfululizo wa Mafundisho ya Papa Franciskco, ambayo tayari yana majina mengine: Tafadhali ombeni kwa ajili yangu, msiachie tumaini lenu kuibiwa na mengine, furaha kuinjilisha, ni vizuri kuwa hapa, kutembea kwenye njia ya amani, Yesu daima anavuta subira kwa ajili yetu, Chemichemi za imani, na tujifunue kwa mwanga wa Bwana.








All the contents on this site are copyrighted ©.