2014-08-07 10:13:34

Shule kuu ya Sheria, Chuo kikuu cha SAUT, Tanzania


Dr. Adelardus Kilangi, Mkuu wa Shule kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino cha Tanzania, SAUT katika mahojiano maalum na Radio Vatican anagusia historia fupi ya Shule kuu ya Sheria na tofauti iliyopo kati ya Shule kuu ya Sheria na Kitivo cha Sheria. Anasema, Shule kuu ya Sheria inakazia zaidi vitendo, kwa kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa vitendo, kuzungumza na kujenga hoja. RealAudioMP3

Shule kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha SAUT imeonesha mafanikio makubwa nchini Tanzania kwa wanafunzi kutoka SAUT wana soko kubwa la fursa ya ajira, kwani ni wanafunzi waliofundwa wakafundika, tayari kukabiliana na changamoto katika uwanja wa sheria. Shule kuu ya Sheria imeonesha mafanikio makubwa pia Afrika Mashariki na kwamba, inaendelea kufanya vyema katika taaluma na tafiti mbali mbali, mambo msingi katika kuwajengea wanafunzi uwezo katika masuala ya sheria.

Dr. Adelardus Kilangi anasema kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na Shule ya sheria wanakaribishwa kwa mikono miwili, lakini watapaswa kuzingatia viwango, uwezo na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa. Ni watu wanaotakiwa kusoma kwa ari kuu, ili waweze kubobema katika taaluma, kwa kuzingatia: kanuni maadili na viwango.

Dr. Adelardus Kilangi anawahimiza wadau mbali mbali katika mfumo wa sheria na wananchi wote kwa ujumla kuendeleza utawala wa sheria, kwa kuzingatia haki msingi za binadamu, ili kukuza kudumisha amani, upendo na mshikamano kati ya watu, kwani bila haki, amani na utulivu, maendeleo ya mwanadamu yako mashakani!







All the contents on this site are copyrighted ©.