2014-08-07 12:28:18

Papa kutangaza wenye heri kadhaa Korea Kusini


Baba Mtakatifu Francisco, hivi karibuni ataanza mfululizo wa ziara za Kimataifa ambamo wiki ijayo ana ratiba ya kutembelea Korea Kusini kwa muda wa siku tano tangu tarehe 13-18 Agosti 2014. Aidha mwezi Septemba atakuwa nia ziara nyingine ya kitume nchini Albania Septemba 21 , 2014, na anatazamia kutembela Sri Lanka kati ya tarehe 15-19 Januari 2015.

Katika ziara ya wiki ijayo kutembelea Korea Kusini , kati ya shughuli muhimu zitakazofanywa na Papa katika ziara hii ni pamoja na kuongoza Ibada ya Misa kwa nia ya kuwataja kuwa wenye Heri Watumishi wa Mungu, Paulo Yun Ji-chung na wenzake 124, katika Ibada itakayofanyika katika uwanja wa GwangHwaMoon. Wafia dini hao wanatajwa kuwa kizazi cha kwanza Wakatoliki Wakorea. Watoto wao tayari walitajwa walikwisha pewa heshima ya kuwa wenye heri katika Ibada iliyofanyika mwaka 1984. Uwanja wa GwangHwaMoon ni mahali pa kihistoria, na ni kituo cha mjini Seoul.

Historia inataja Haemi ni mahali palipofanyika mauaji ya Wakorea 132, ambao wengi wao majina yao hayajulikani, lakini walikamatwa na kuuawa wakati wakikimbilia Naepo kusalimisha roho zao lakini walikamatwa na kuangamizwa kwa sababu ya kukiri imani yao kwa Kristo. Baadhi ya wanafunzi walizikwa wakiwa hai wakati wa mateso ya Mujin 868.

Mahali mauaji hayo yalipofanyika pamekuwa leo hii sehemu ya sala kwa kumbukumbu ya mateso na mauaji ya waamini, pakijulikana kama kijiji cha Kkottongne ( Kijiji cha maua ) kilicho anzishwa mwaka 1976 na Padre Oh Woong Jin, ambaye aliamua kujenga "Nyumba ya Upendo" baada ya kuona upendo wa kina wa muumini mmoja, Gwi Dong Choi, akitoa chakula kwa watu maskini na walemavu wapatao 18. Padre Oh Woong Jin, aliguswa na huduma hiyo na kuanzisha kituo rasmi cha kutoa msaada kwa maskini wasiojiweza , walemavu , wasio kuwa na makazi na hata walevi wa kupindukia. Uzoefu wa Kkottongne ulivuka mipaka , na kutawanyika katika mataifa mengine kama Bangladesh, Philippines, Uganda, Haiti, India, Canada na Marekani.

Huduma hii muhimu katika kijiji hiki, hutegemea michango na misaada kutoka kwa waamini na pia msaada wa serikali. Na kwa wakati huu kinaendeshwa na Shirika la Masita wa Yesu wa Kkottongne wapatao 211. Pia kunaShirika la Ndungu (Brothers)wa Yesu wa Kkottongne wapato 65, na husaidiwa na watu wa kujitolea wapatao 1,000 ambao hupeana zamu kufanikisha shughuli za kijiji hiki ambach kwa sasa kina uwezo wa kuhifadhi watu 5,000, watu waliopoteza tumaini , walemavu na waliotelekezwa na familia zao. Kituo hiki cha Kkottongne pia hujulikana kama Nyumba ya Malaika kutokana na huduma zake kuwa nzuri. Ndani ya kijiji mna shule ambapo watoto walemavu waliotelekezwa na familia zao kwa sababu ya ulemavu wao huweza kujifunza kwa wakiwa 121.

Kardinali Ferdinando Filoni, Mkuu wa shirika kwa ajili ya UInjlishaji mpya, anaielezea historia ya Kanisa Katoliki Korea na upendo wake wa kimisionari udhahiri katika matendo ya walei, yanayotoaa sura kamili ya Kanisa katika ujumbe wake wa kudumu, kama ilivyo ainishwa katiak Waraka wa Kitume wa Papa Francisco, wa Fraha ya InjiliGaudium Evangelii. Haya alieleza wakati wa na gazeti la “Vatican Insider"juu ya ziara ya Papa Francisco hivi karibuni Korea ya Kusini, ambako Papa atawataja kuwa wenye Heri waamini 124, waliouawa kwa kushupalia kikamilifu imani yao. Kardinali anaelezea kama mashahidi hao wa imani , inakuwa ni ishara ya kutia moyo, katika kukumbuka pia kwamba, katika nchi mbalimbali dunani , Papa ana nafasi yake. Na hivyo kuna matumaini kwamba , ipo siku, Mkuu wa Kanisa la Ulimwengu pia ataweza kutembelea hata China.








All the contents on this site are copyrighted ©.