2014-08-06 10:20:04

Rais Kenyatta apiga rufuku uuzaji wa ardhi Lamu!


Serikali ya Kenya imeamua kutaifisha asilimi 70% ya ardhi ya Lamu, eneo maarufu sana kwa shughuli za utalii kutokana na mauzo yake kufanywa kinyume cha sheria. Uamuzi huu umetolewa na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya baada ya mashambulizi ya kigaidi kuzidi kujitokeza kwenye mwambao wa Kenya na hivyo kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao.

Vyombo vya sheria nchini Kenya vimegundua kwamba, mashirika 22 ya kigeni yamenunua ardhi eneo la Lamu kinyume cha sheria kati ya mwaka 2011 hadi mwaka 2012. Vitendo vya kigaidi vilivyowahusisha hata baadhi ya viongozi wa serikali za mtaa pamoja na migogoro ya ardhi ni kati ya mambo ambayo yamechochea mashambulizi kwa watu wasiokuwa na hatia.







All the contents on this site are copyrighted ©.