Kuweni mwanga na chumvi ya Dunia Papa awaasa vijana
Baba Mtakatifu Francisko Jumanne jioni, alikutana na watumishi wa altareni, wapatao
50,000 kutoka Ujerumani na nchi jirani ya Uswiss na Austria. Vijana hao, wenye umri
kati ya miaka 13 -27, kila mwaka huwa na ratiba ya kufanya hija katika Madhabahu Matakatifu
yaliyoko jijini Roma na Vatican. Kwa mwaka huu, hija yao imeongozwa na kauli mbiu:
"Ni huru sababu ni halali kutenda mema".
Baba Mtakatifu alikutana na vijana
hawa katika uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, walioufanya uwanja huo kuwa
hai na sura ujana, ukipambwa zaidi na muziki hai wa kisasa. Papa baada ya kuwazungukia
vijana akiwa katika gari lake la Kipapa, aliwasalimia na kufurahi pamoja nao . Na
kisha aliongoza Ibada ya Masifu ya Jioni , na kuwahutubia kwa lugha ya kijerumani,
ambamo hotuba yake ililenga katika kufafanua somo kutoka waraka kwa Wagalatia, maneno
ya Mtakatifu Paulo “ punde tu tumesikia ... kuvutia mawazo yetu. Wakati umetimia”.
Papa
Francisco alifafanua maneno: sasa ni wakati, Wakati Mungu amekamilisha kazi yake.
na kufafanua kuwa maneno haya yanatuonyesha sisi kwamba, Yeye ni Baba Mwema, kupitia
Umwilisho wa Mwana, ambaye anakuwa mmoja wetu. Kwa ufahamu huu wa mtu halisi katika
jina la Yesu, tunaweza kuelewa nini maana ya Mungu kweli. Yeye anataka kumweka huru
binadamu , ili kwamba daima aweze kujisikia salama kama mtoto wa Baba Mwema.
Lakini,
Papa alisema,” kuufanikisha mpango huu, Mungu alihitaji mtu binadamu, mwanamke ,
Mama kumleta Mwanae duniani. Na mwanamke huyo ndiye Bikira Maria, ambaye tunamheshimu
katika Ibada hii”. Papa Francisco aliendelea kueleza kwamba , Maria alikuwa huru kabisa.Na
katika uhuru wake alichagua kusema" ndiyo" kwa mpango wa Mungu, alisema ndiyo katika
kutenda mema. Na hivyo ndivyo yeye alivyochagua kumtumikia Mungu. Alimtumikia Mungu
na binadamu. Kwa maelezo hayo Papa aliwahimiza watu wote kuiga mfano wa Bikira
Maria, kama wanataka kujua kile Mungu anatarajia kutoka kwao kama watoto wake.
Baada
ya Ibada hii ya Kiliturujia, Papa Francisco , alizungumza na vijana kupitia njia ya
maswali na majibu. Alijibu maswali kadhaa kutoka vijana hao watumishi wa altareni.
Akijibu moja ya swali alisema dunia, inahitaji watu wa kushuhudia wengine kwamba,
Mungu anatupenda, kwamba hakika Yeye ndiye Baba yetu, na vijana wana nafasi ya pekee
ya kuwa mashahidi wa hilo katika hija hii ya maisha. Na kwamba Vijana wameitwa na
Yesu na wanatakiwa kwa uhuru kabisa kutoa jibu lao, si tu ndani mwao, au parokiani
au katika vyama vyao , lakini hasa kwa wale wanaoonekana kuwa mbali na Mungu.
Papa
Francisko alionyesha kutambua matatizo ya vijana wengi katika uzoefu wao wa kutunza
ahadi yao ya kuendelea kuhudumia Kanisa na shughuli nyingine mbalimbali na kuwatia
moyo kwamba, mara nyingi matatizo ni changamoto muhimu katika utamaduni wa makuzi
ya binadamu. Na hufundisha mtu kujipanga vyema. Papa aliwasifu vijana hao wa Kijerumani
kwamba , wao wanafanya vyema katika hili. Na kwamba kati miongoni mwa mahitaji mengi
ya kawaida ya kila siku, Papa alisema, ni muhimu na lazima kutoa vipaumbele kukumbuka
kwamba Muumba wetu, ndiye anayetupatia maisha, anatupenda, na huambatana nasi katika
hija yetu ya maisha.
Mwisho Papa alirejea Mada ya mwaka huu ya Hija ya
Vijana , akisema tumepokea kutoka kwa Mungu zawadi ya uhuru, kwa sababu, tumeumbwa
kwa sura na mfano wake. Na kama uhuru huu ukitumiwa vibaya, unaweza kuwa sababu
ya kuwa mbali na Mungu, na kutufanya tupoteze hadhi yetu ya kufanana naye aliyotuvalisha
sisi. Na ndiyo maana tunahitaji miongozo na sheria, katika jamii na katika kanisa
: kutusaidia kufanya mapenzi ya Mungu, na hivyo kuishi kulingana na heshima na hadhi
ya kwua watoto wa Mungu.
Baba Mtakatifu aliwasihi vijana wasitumie vibaya uhuru
wao ! Wasipoteze hadhi kubwa ya kuwa watoto wa Mungu, waliyopewa bure! Na kama
wataandamana na Yesu na Injili yake, uhuru wao, unakuwa kama mmea unaochanua maua
na kuzaa matunda mazuri tele! Kwa kutembekea katika njia hiyo ya Yesu, wataweza kutapata
furaha halisi, sababu Yeye anataka wawe wanaume na wanawake wenye furaha kamilifu.
Ni tu kaika kushikamana na Mapenzi ya Mungu , tunaweza kufanya yaliyo mema na kuwa
mwanga na chumvi ya dunia.