Baba Mtakatifu Francisco amepeleka salaam za rambirambi kwa Askofu Mkuu Peter Comensoli
, Mtawala wa kitume wa Jimbo kuu la Sydney Australia, kufuatia kifo cha Kardinali
Edward Beda Clancy , kilichotokea majira ya saa tano za asubuhi Jumapili iliyopita.
Katika rambirambi hizo, Papa kwa moyo wa dhati wa kibaba, amesema, yupo pamoja
na Askofu Mkuu Comensoli, na waamini wote wa jimbo kuu la Sydney. Na anaungana nao
katika sala za kuiombea roho marehemu Kardinali Edward Clancy ipokelewe kwa Mungu,
Baba wa rehema, kwa moyo wa shukrani kwa miaka yake ya huduma ya kiaskofu, na hekima
zake za kichungaji kwa wakati wa uongozi wake katika Jimbo Kuu la Sydney, katika
kujali mahitaji ya maskini,na msaada wake kwa ajili ya elimu Katoliki na kiekumeni
na maono yake katika mtazamo mpana wa uraia.
Baba Mtakatifu ametoa baraka
zake kwa wote , watakao shiriki katika Ibada ya Misa ya Wafu na Mazishi na wote
wanao omboleza na kuguswa kwa namna ya kipekee na kifo cha Kardinali Clancy, waweze
kuomboleza katika tumaini la ufufuo wa Kristo na ahadi ya uweza na faraja katika
Bwana.