Papa kutembelea Sri Lanka na Ufilippini, Januari 2015
Baba Mtakatifu Francisko amekubali mwaliko uliotolewa na Serikali na Baraza la Maaskofu
Katoliki Sri Lanka na hivyo, atatembelea nchini Sri Lanka kuanzia tarehe 12 hadi tarehe
15 Januari 2015.
Wakati huo huo, Baba Mtakatifu Francisko amekubali pia mwaliko
wa kutembelea nchini Ufilippini kuanzia tarehe 15 hadi tarehe 19 Januari 2015. Taarifa
inaendelea kuonesha kwamba, Vatican kwa siku za usoni, itatoa ufafanuzi zaidi wa hija
hii ya kitume ya Baba Mtakatifu Barani Asia!