2014-07-28 10:16:32

Abiria waliofariki kwa ajali ya ndege huko Mali wakumbukwa kwa Ibada!


Baraza la Maaskofu Katoliki Burkina Faso, Jumapili tarehe 27 Julai 2014 katika Kanisa kuu la Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili, Jimbo kuu la Ouagadougou, limeadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kuwakumbuka na kuwaombea abiria wa Shirika la Ndege la Algeria iliyoanguka hivi karibuni nchini Mali na hivyo kusababisha vifo vya abiria 116 waliokuwemo ndani ya ndege hiyo! Ibada hii ya Misa Takatifu imeongozwa na Kardinali Philippe Ouedraogo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Ouagadougou, Burkina Faso.

Katika Ibada hii waamini pia wamewakumbuka na kuwaombea ndugu, jamaa na marafiki wa abiria waliofariki dunia kwa ajili ya ndege huko Mali na sehemu nyingine za dunia ambako hadi sasa watu wanaendelea kuomboleza kutoka na majanga ya ajali za ndege. Ni katika ukimya, watu wanaweza kupata majibu yanayoendelea kusumbua vichwa vya watu wanapotafakari kuhusu ajali hizi za ndege. Ni Mwenyezi Mungu peke yake anayeweza kuzima kiu ya mahangaiko ya mwanadamu, changamoto kwa waamini kuendelea kujikita katika imani na matumaini wakati huu wa maombolezo na msiba mkubwa.







All the contents on this site are copyrighted ©.