Padre Federico Lombardi msemaji mkuu wa Vatican anafafanua kwamba, hadi sasa Baba
Mtakatifu Francisko amepata mialiko mingi nchini Marekani na bado inafanyiwa kazi.
Kuhusu ushiriki wa Baba Mtakatifu Francisko kwenye maadhimisho ya Siku ya Nane ya
Familia kimataifa itakayoadhimishwa Jimbo kuu la Philadelphia, Marekani kunako mwaka
2015, Padre Lombardi anawasihi waamini kuvuta subira, watajulishwa kwa wakati muafaka!
Hadi
sasa Baba Mtakatifu Francisko ameonesha utashi wake wa kushiriki katika maadhimisho
ya Siku ya Nane ya Familia Kimataifa, lakini hadi sasa hakuna mchakato ambao umekwishaanzishwa
kwa ajili ya safari hii ya kitume nchini Marekani au Mexico, kama ambavyo baadhi ya
waandishi wa habari walivyotaka kufahamu. Bado kuna mwaka mzima, kabla ya tukio hili
kuadhimishwa huko Philadelphia, Marekani!