2014-07-25 12:19:52

Askofu mkuu Souraphiel achaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa AMECEA


Wajumbe wa mkutano mkuu wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki na kati, AMECEA katika mkutano wake wa kumi na nane uliokuwa unaongozwa na kauli mbiu "Uinjilishaji kwa njia ya wongofu na ushuhuda wa imani ya Kikristo", wamemchagua Askofu mkuu Berhaneyesus D. Souraphiel wa Jimbo kuu la Addis Ababa, nchini Ethiopia kuwa Mwenyekiti mpya wa AMECEA. Askofu mkuu Souraphiel anachakua nafasi ya Askofu mkuu Tarcisius Zizaye wa Jimbo kuu la Lilongwe, Malawi aliyemaliza muda wake.

Askofu mkuu Souraphiel alipadrishwa kunako tarehe 4 Julai 1976. Akawekwa wakfu kuwa Askofu kunako mwaka 1998 na kunako tarehe 7 Julai 1999 akateuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Addis Ababa kwa kumrithi Kardinali Paulos Tzadua aliyekuwa analiongoza Jimbo kuu la Addid Ababa, Ethiopia.







All the contents on this site are copyrighted ©.