2014-07-24 15:31:51

Papa ajiunga katika maombelezo ya Taiwan


Baba Mtakatifu Francisko , mara baada ya kupewa taarifa za ajali ya ndege iliyoaguka karibu na uwanja wa ndege wa Magong Taiwan, siku ya Jumatano, k alipeleka salaam za rambirambi kwa familia zote za wahanga wa ajali hii. Na aliwahakikishia sala na maombezi yake kwa ajili ya wote walioathirika na janga hili. Juu ya yote, anawaombea baraka na faraja, nguvu na amani ya Bwana wa uzima wa milele.

Salaam hizi, zilitumwa kwa niaba ya Papa na Kardinali Piero Parolin, Katibu wa Vatican, kwa Askofu Mkuu John HUng Shan Chuan wa Jimbo Kuu la Tapei , na Rais wa Baraza la Maaskofu Kanda ya China.

Jumatano ndege ya Shirika la Ndege la Taiwan, ikiwa na watu 58, kati ya wakiwa wasafiri 54 na wafanyakazi wa ndege, ilianguka wakati ikijaribu kutua ghafla katika uwanja wa Magong. Kati ya wasafiri hao 47 walifariki papo hapo na wengine kunusulika ambao wengi wao hali zao zinatajwa kuwa ni mbaya . Chanzo cha ajali hiyo ni hali mbaya ya hewa, iliyoandamana kibunga kikali, mvua kubwa na upepo mkali. Hali iliyofanya hata shule na maeneo ya biashara katika mji huo kufungwa kwa muda. Ndege hiyo ilikuwa katika safari zake za kawaida kati ya mji wa Kahohsiung na kisiwa cha Penghu.








All the contents on this site are copyrighted ©.