Baraza la Maaskofu Katoliki Afrika ya Kusini kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu
ya Wayesuit, Jimbo kuu la Johanesburg, wameandaa onesho la vyombo vya mawasiliano
ya Kanisa Afrika ya Kusini. Onesho hili ambalo litafanyika Jumamosi tarehe 26 Julai
2014 linaongozwa na kauli mbiu "Njoo ukuze vipaji vyako vya mawasiliano".
Walengwa
wakuu ni wanafunzi wa shule za sekondari, taasisi za elimu ya juu pamoja na vyuo vikuu
nchini Afrika ya Kusini, bila kuwasahau wadau katika ulimwengu wa mawasiliano ya Jamii
kutoka katika Majimbo na Parokia mbali mbali mbali nchini Afrika ya Kusini.
Vyombo
vya mawasiliano ya Jamii vinavyomilikiwa na kuendeshwa na Kanisa Katoliki Afrika ya
Kusini, vitafanya onesho ili kuwashirikisha waamini na watu wote wenye mapenzi mema
uzoefu na mang'amuzi ya Kanisa katika mchakato wa Uinjilishaji Mpya. Hawa ni watu
wanaofanya kazi katika mitandao ya kijamii, Radio, Luninga, Magazeti na Majarida mbali
mbali. Watu watakaoshiriki katika onesho ili ambalo pia linaweza kuwa ni msaada mkubwa
kwa vijana kutambua na hatimaye kukuza vipaji vyao, watafundishwa nadharia asubuhi
na jioni, wataweka katika vitendo yale waliyojifunza!