2014-07-11 10:29:08

DRC haina mpango wa kuchakachua Katiba!


Serikali ya DRC imekanusha uwepo wa mchakato unaotaka kufanya mabadiliko katika Katiba ya Nchi ambayo kimsingi ni sheria mama ili kumwezesha Rais Joseph Kabila kuwania tena madaraka katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika nchini humo mwaka 2016.

Itakumbukwa kwamba, Baraza la Maaskofu Katoliki DRC liliona kwamba jitihada zozote za kutaka kufanya marekebisho katika Katiba zinaweza kutibua mustakabali wa wananchi wa DRC. Maaskofu wanataka kuona uchaguzi nchini humo unakuwa: huru, kweli na haki. Ni wajibu wa wanasiasa kusimamia mafao ya wengi, ustawi na maendeleo ya wananchi wa DRC.









All the contents on this site are copyrighted ©.