2014-07-10 07:45:10

Papa Mfukoni mwako...


(Vatican Radio / PCCS) Baba Mtakatifu Francisco, ameonyesha kufurahia juhudi za vyombo vya mawasiliano Vatican katika huduma zake za kuimarisha uwepo wa vyombo hivyo katika ulimwengu wa digital. Papa alionyesha furaha hiyo, siku ya Jumatatu,wakati akitazama toleo la ukurasa mwingine mpya, katika simu ya mkononi “lilioitwa “The Pope App", kama ilivyobuniwa na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mawasiliano Jamii.

Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mawasiliano Jamii, Askofu Mkuu Claudio Celli, akifuatana na mratibu wa juhudi hizo, Thaddeus Jones, walikutana na Papa kuonyesha sifa za ukurasa huo, ambao tangu tarehe 4 Julai ulianza kupatikana katika mitandao ya iTunes na Google, katika lugha tano. Pope App 2.0 inapatikana bure na inaweza kunakiriwa bure au kuchotwa bure kwenye vifaa Apple na Android. Na kwa kuwezeshwa na News.va, inatoa taarifa na habari za hivi karibuni juu ya Papa, kama zinavyo tolewa na vyombo vya habari vya Vatican ikiwemo Vatican Radio.

Lengo la mradi huu ni kurahisisha zaidi upatikanaji wa habari sahihi za Vatican. Askofu Mkuu Celli, alieleza na kuongeza pia inaruhusu watu kuwa karibu zaidi Papa, katika huduma yake ya kichungaji na ujumbe wake wa upendo wa Mungu.

Akizungumza na Gazeti la L’0sservatore Romano juu ya Juhudi katika mtazamo kutunza jadi na ubunifu mpya , katika ulimwengu wa Mawasiliano , anasema, katika hatua kubwa za maendeleo makubwa katika mawasiliano ya digital, "Kanisa kwa wakati huu, kwa hakika haliwezi kujitenga na kubaki katika mawasiliano ya jadi ya redio, televisheni na magazeti. Ni hakika Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mawasiliano ya Jamii, aliendelea kueleza, Kanisa haliwezi kufungia nje hatua za maendeleo katika njia hii ya mawasiliano, ingawa haina maana kupoteza hisi zake za nguvu , katika uwajibikaji wa kutunza uadilifu katika mazingira ya teknolojia mpya.

Na ndiyo maana, pamoja na Papa Francisco, kuendelea kuonyesha kuwa karibu sana na mfumo wa jadi wa mawasiliano, pia hajiweki mbali na mifumo ya sasa katika mawasiliano jamii . Yeye anapenda kuzungumza na watu, katika kila uwezekano, hata mawasiliano ya simu moja kwa moja kwa wahusika badala ya kutegemea tu weledi wa maelezo katika mtandao; na hajaacha utamaduni wa kuandika barua kwa mkono wake mwenyewe. Lakini pamoja na hilo, hutumia njia za kisasa kama kutuma ujumbe kwa makundi ya watu, ambao huonana nao ana kwa ana kupitia mtandao wa video , ambayo hutoa nafasi za kusikilizana na kubadilishana mawazo kama vile wako sehemu moja. Na pia muda wote yuko tayari kuzungumza na waandishi wa habari, vyombo vya habari, magazeti au mitandao ya televisheni, na huwa tayari kufanya mahojiano, na hajamkatalia mtu yeyote.

Maneno ya Papa daima ni wazi, halisi na moja kwa moja na si ya mkato wala kuzunguka mbuyu. Na huheshimu mahojiano hasa na wazee ambao pengine kwao si rahisi kuikubali teknolojia mpya au kutumia vifaa vya kisasa au lugha ya tarakimu katka ulimwengu wa mitandao ya kijamii. Watu ambao bado wanathamini zaidi habari zilizochapishwa katika magazeti, au kutangazwa katika redio na televisheni. Lakini pia Kanisa haliwezi kubaki limejifungia tu katika njia hizo za kijadi, kwani ni muhimu likatembea pamoja na teknolojia Mpya. Na Papa Francisco anajua na anaruhusu hilo, ameeleza Askofu Mkuu Celli katika mahojiano na gazeti la L'Osservatore Romano.








All the contents on this site are copyrighted ©.