2014-07-08 09:22:17

Tume ya kutetea watoto dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia yakutana Vatican


Tume ya Kipapa kwa ajili ya Ulinzi wa Watoto dhidi ya manyanayso ya kijinsia, ilifanya kikao chake Jumapili hadi Jumatatu ( 6-7Julai 2014 ), katika jengo la Domus Sanctae Marthae, chini ya uratibu wa Kardinali Sean Patrick O'Malley, OFM Cap., Kwa kushirikiana na Msgr. Robert Oliver .

Padre Federico Lombardi, Mkuu wa Ofisi ya Habari ya Vatican, akitoa muhtasari wa kikao hicho cha siku mbili , alitaja kikao hicho kilifanya majadiliano yake kwa kuzingatia mada zifuatazo :
- Mapendekezo kwa ajili ya uchaguzi na uteuzi wa wajumbe wapya , kwa lengo la kuishirikisha tume katika uwakilishi mpana zaidi kutoka maeneo mbalimbali ya kijiografia.
- Katiba ya Tume.
- Haja ya kuanzisha ofisi za utendaji za Tume.
- Uwezekano wa kuandaa vikundi kazi juu ya mada maalum kwa kushirikiana na
ya wataalamu na taasisi nyingine.


Kikao kilikamilika kwa kutaja kikao kijacho , kitafanyika mwezi wa Oktoba. Ni matumaini ya Tume kwamba wajumbe wapya walio chaguliwa au kuteuliwa wataweza kuhudhuria kikao . Aidha kikao hicho, kilitoa angalisho maalum katika maandalizi ya wahanga kadhaa wa madhulumu ya kinjisia yaliyofanywa na viongozi wa Kanisa, kukutana na Papa Francisco, kama ilivyokuwa imepangwa.

Wahanga hao waliowasili katika nyumba ya wageni ya Mtakatifu Marta ya mjini Vatican, wakati wa mlo wa mchana, Papa alijitokeza na kuwasalimia kwa hotuba fupi . Wahanga hao walikuwa ni watu wazima sita , wanaume watatu na wanawake watatu, kutoka UjerumanI , Ireland, na Uingereza, na kila mwathirika alikuwa amesindikizwa na familia yake au rafiki yake.


Tukio hili ni mwaliko uliotolewa na Cardinal O'Malley kwa nchi kadhaa ambapo Kanisa limeunda mfumo maalum kuhusu waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia. Na Washiriki waathirika walipewa mwaliko wa kukutana na Papa. Mapema Jumatatu Papa alitolea Ibada ya Misa kwa ajili yao katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marthae, na wahanga walihudhuria pia na wote waliokuwa wameandamana nao, pia wajumbe wa Tume kwa ajili ya ulinzi wa watoto, na idadi ndogo ya waamini wengine. Nia kuu ya Ibada hiyo ikiwa kwa ajili ya haki na amani.


Baada ya Misa, Papa alisalimu kila aliyeshiriki katika Ibada hii . Baada ya kifungua kinywa, Papa , alifanya a majadiliano binafsi katika chumba cha faragha ndani Jengo la Domus Sanctae Marthae na kila mhanga akiwa na wale walioandamana naye , mmoja baada ya mwingine. Majadiliano yaliyodumu ilidumu tangu saa tatu hadi saa sita na nusu za mchana.


Washiriki, baada ya majadiliano, walionyesha hisia zao na kuridhika baada ya kusikilizwa na Papa na jinsi alivyoonyesha kujali na tahadhari inayotolewa . Papa alionyesha wazi kwamba, kumsikiliza mtu, husaidia kuelewa na kuandaa njia ya kurejesha imani, kuponya majeraha, na kufungua uwezekano wa maridhiano na Mungu na Kanisa.









All the contents on this site are copyrighted ©.