lLifuatalo ni Tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania kwa Bunge Maalum la Katiba
nchini Tanzania lililotolewa na Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la
Maaskofu Katoliki Tanzania alipokuwa anazungumza na vyombo vya habari Jijini Dar es
Salaam. TAMKO LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA KWA BUNGE MAALUMU LA KATIBA (BMK)
UtanguliziKatika
ujumbe wetu wa Kichungaji wa Pasaka 2014, sisi Maaskofu Katoliki Tanzania, tuliwaandikia
barua watu wote wenye mapenzi mema kwa nchi yetu tukiwaalika kuchukulia maanani mchakato
wa kuandika Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wakati huu tunawaalika
Watanzania wote kwa pamoja, tuungane kuwakumbusha wale waliopewa dhamana ya kukamilisha
Rasimu ya Pili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kuwajibika binafsi na katika maridhiano
kutupatia Katiba maridhawa. Tunawaasa tukiwaombea dhamiri zao zipate maono mapya,
waweze kubeba kiaminifu dhamana hiyo walio kabidhiwa.
Waheshimiwa Wajumbe wa
Bunge Maalumu la Katiba,
Kwa moyo wa Sala na tafakari makini tulifuatilia mlivyojadiliana
katika BMK kuanzia mwezi Februari hadi Aprili 2014. Katika siku sitini na saba (67),
ninyi wateule wa Rais mpatao mia sita (600), mlijadiliana pasipo umoja, mkishambuliana
kwa kauli kali kati yenu, mkikashifiana pasipo udhibiti wa uongozi mliojichagulia
wenyewe kwa kanuni na sheria mlizojitungia. Mwenendo huo ulikuwa wa kusikitisha na
kuchukiza katika mahali pale panapoheshimiwa na wote.
Tulitegemea majadiliano
katika kuheshimiana hoja za kizalendo na kiungwana zitokanazo na mambo na masuala
makuu yaliyopendekezwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba. Badala yake tulijionea mabishano
makali na mpasuko uliosababisha upotoshaji wa nia iliyokusudiwa. Hatimaye hila na
gilba zikateka kabisa jukumu adili la BMK.
Tukumbuke Rais wa Jamhuri wa Muungano
wa Tanzania kwa uthubutu na ujasiri wa kipekee, alianzisha mchakato wa kuunda Katiba
Mpya, na kisha aliridhia kwa kuipokea rasmi kwa furaha Rasimu ya II ya Tume ya Mabadiliko
ya Katiba. Ni lazima sasa tujiulize, nini kimetokea hadi kugeuza kabisa mwelekeo mzima
wa mchakato wa Katiba kwa kuikejeli na kuishutumu vikali Rasimu hiyo katika wakati
wa kipekee kabisa wa kihistoria wa uzinduzi wa BMK? Hata kusahau gharama kubwa ambayo
ilibebwa na walipa kodi? Na sasa hali inaonyesha dhahiri jambo hili limeiingiza nchi
kati ka mgogoro mkubwa unaoashiria hatari mbeleni.
Mwaliko kwa wahusika wote
kuwa na utashi wa kisiasa
Kwa maoni yetu, tatizo hill kubwa ambalo limekuwa
kikwazo kikubwa linaonyesha kukosekana utashi wa kisiasa na wahusika kutokuwa wakweli
juu ya suala zima la Mchakato wa Katiba.
Tunawaomba wajumbe wa BMK kuwa wamoja
na kufanya kazi yenu kwa mtazamo usioegemea siasa za vyama. Kuandika Katiba ni kazi
iliyo ngazi ya juu zaidi ya siasa za vyama, na hivyo utashi wa kisiasa wa kuunda Katiba
Mpya kwa kuzingatia Rasimu II utaweza kuridhiwa kwa kuzingatia msingi huu.
Kwa
kadiri ya hali ya nchi yetu ziko sababu za kutosha za kutaka Katiba Mpya. Sababu hizi
ni pamoja na ufisadi, wananchi kujisikia kukosa usalama, nchi kutokuwa na dira, tunu
msingi n.k.
Ni kwa hiyo, tunawasihi kwa mara nyingine tena ninyi wajumbe wa
BMK kurejea katika sehemu ya pill ya mjadala hapo mwezi Agosti mkiwa na moyo na mtazamo
mpya. Tunawaomba achaneni kabisa na ubinafsi, uwe wa mtu mmoja mmoja, ama katika vikundi.
Kwa kazi yenu tusaidieni sisi watanzania tuweze kujivunia kuwa na Taifa adilifu tukifanya
kazi kwa pamoja kwa ajili ya manufaa na ustawi wa wote. Kumbukeni BMK mnao wajibu
wa kimaadili kwa nchi yenu na vile vile kwa namna mnavyotekeleza wajibu wenu mnaandika
historia ya nchi yetu. Wajibu wa Kimaadili Kubeba dhamana ya kuandaa Katiba
Mpya ni wajibu wa kimaadili kwenu. Tambueni kwamba Watanzania hawako tayari kurudi
nyuma na kuendelea na maisha yanayoongozwa na Katiba ya 1977, kwa sababu licha ya
mapungufu yake na ukiukwaji mkubwa ambao umekuwa ukifanyika, kufanya hivyo (kuendelea
kuongozwa na Katiba ya 1977) kutaleta migogoro mikubwa yenye kuhatarisha vikali amani
nchini.
Wajibu miiokabidhiwa ikiwa mtautimiza kwa dhamira njema, mtalijengea
taifa letu msingi imara, uliosheheni tunu za kimaadili ambazo ni heshima katika utu
wa mwanadamu, umoja, mshikamano na kujali manufaa na ustawi wa wote. Ni lazima matunda
ya kazi yenu yawe ni kulipatia taifa dira inayowapa watu msukumo wa kujenga pamoja
taifa Ienye watu wamoja na wanaojaliana kwa stahamala katika tofauti zao. Wajibu wenu
huo ni Mtakatifu, na hivyo ni kosa kubwa mno kuusaliti kwa sababu ya ushindani katika
medani za kisiasa au kujitafutia sifa mbele ya watu.
Jukumu la Kihistoria
Kwa
matokeo yoyote yatakayotokana na kazi yenu katika BMK, Watanzania watawawajibisha.
Ikiwa matokeo yatakuwa yenye kuleta mema, na kuimarisha amani na utulivu nchini, watu
wote watawashukuru na kuwasifu. Lakini kama tunda la kazi yenu litakuwa ni Ienye kuingiza
nchi katika matatizo zaidi, kuwataabisha wananchi na kukosa maelewano baina yao, basi
watu watawahukumu na kuwawajibisha kwa kukosa umakini katika jukumu hili muhimu mlilokabidhiwa.
Kwa
sasa tunahitaji Katiba itakayowezesha ushiriki kamili wa watu katika maamuzi ya vipaumbele
vya maendeleo yao na ya Taifa. Ni Katiba shirikishi katika matumizi ya madaraka, iii
yatumike kwa ajili ya kuhudumia wote, badala ya wachache. Tunahitaji Katiba ambayo
inaruhusu utawala wa sheria, haki sawa kwa wote, manufaa na ustawi kwa wote na kuheshimu
UTU wa kila mmoja. Ni Katiba iwezayo kuzuia matumizi mabaya ya madaraka na ufisadi.
Hicho ndicho wananchi wanachokitarajia kutoka kwenu. Yeyote anayedharau hitaji
la Katiba mpya ama anayejaribu kupuuza na kuweka kando Rasimu II, huyo sio mwakilishi
wa utashi wa watu. Mwisho wake historia itamhukumu vikali mtu huyo.
Wajumhe
wa K, msiwaangushe watu wenu.
Hitimisho
Sisi Maaskofu Katoliki Tanzania
tunawaahidi Sala zetu iii Mwenyezi Mungu awaangazie Nuru yake na kuwajalia nguvu ya
kiMungu muweze kukamilisha kazi kwa mafanikio, kadiri ya matarajio ya watu wake wa
Tanzania.
Tunawaalika watu wote wenye mapenzi mema kuwaombea wajumbe hao wa
Bunge Maalum la Katiba wajaliwe neema za Mungu.