Sr. Melone ateuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kipapa!
Profesa Mary Melone, mtawa mwenye umri wa miaka 50 ameteuliwa kuwa ni Mkuu wa Chuo
Kikuu cha Kipapa cha Antonianum kilichoko mjini Roma. Huyu ni mtawa kutoka Shirika
la Wafranciskan ambaye anaweka historia ya kuwa ni mtawa wa kwanza kuteuliwa kuongoza
Chuo Kikuu cha Kipapa. Ni mtaalam wa masuala ya elimu na taalimungu katika mafundisho
tanzu ya Kanisa.
Ni Jalimu aliyebobea na kwa miaka kadhaa amefundisha chuoni
hapo na ni mwandishi wa vitabu, majarida na makala mbali mbali. Mtawa aliyebobea katika
kuhariri vitabu mbali mbali. Professa Melone atakiongoza Chuo Kikuu cha Kipapa cha
Antonianum kuanzia mwaka 2014 hadi mwaka 2017.