2014-07-05 16:09:15

Waomba ulinzi kutoka Umoja wa Mataifa!


Wananchi wa Nigeria wanaoishi Kaskazini mwa nchi hiyo ambao kwa miaka kadhaa wanakabiliana na mashambulizi pamoja na vitendo vya utekaji nyara vinavyofanywa na Kikundi cha Boko Haram, wameomba ulinzi kutoka Umoja wa Mataifa. Mjini Chibok, wanafunzi zaidi ya mia mbili walitekwa nyara hadi sasa hawajulikani waliko.

Wananchi wanasema, Serikali kuu imeshindwa kuwahakikishia wananchi wanaoishi Kaskazini mwa Nigeria ulinzi na usalama ndio maana wanauomba Umoja wa Mataifa kuwasaidia kwa kuwapatia ulinzi na usalama dhidi ya mashambulizi yanayofanywa na Kikundi cha kigaidi cha Boko Haram.

Takwimu zinaonesha kwamba katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita watu zaidi ya mia mbili wameuwawa kikatili kutokana na mashambulizi kumi na tano yaliyofanywa kwenye vijiji kadhaa Kaskazini mwa Nigeria.







All the contents on this site are copyrighted ©.