Baba Mtakatifu Francisko, Jumanne, tarehe 1 Julai 2014 alijumuika na Baraza la Makardinali
wanane katika mkutano wao wa tano unaojadili marekebisho msingi katika Sekretarieti
ya Vatican. Hili ni Baraza la Makardinali alilolichagua ili kumsaidia kutekeleza utume
wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro kwa kuzingatia ushauri na maelekezo yaliyotolewa
na Makardinali wakati wa mikutano yao elekezi.
Baba Mtakatifu Francisko pamoja
na Makardinali wataendelea na mkutano wao hadi tarehe 4 Julai 2014. Itakumbukwa kwamba,
Makardinali hawa waliwahi kufanya mikutano yao, tarehe 1- 3 Oktoba 2013; tarehe 3-
5 Desemba 2013; tarehe 17-19 Februari 2014.