Askofu mkuu Alfred Adewale Martins wa Jimbo kuu la Lagos, Nigeria katika ujumbe wa
matashi mema kwa waamini wa dini ya Kiislam, katika kipindi hiki cha Mfungo Mtukufu
wa Mwezi wa Ramadhani, anawaalika wanapofunga na kujinyima, wawakumbuke maskini na
wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii.
Hiki ni kipindi ambacho wanaweza
kufanya tafakari ya kina kuhusu upendo kwa Mungu na jirani pamoja na kukazia umuhimu
wa watu kuishi katika msingi ya haki na amani, kwa kuheshimiana na kuthaminiana kama
watoto wa Mwenyezi Mungu licha ya tofauti zao za kidini na kiimani.
Ni mwaliko
kwa kushikamana na kusaidiana na watu wote wenye mapenzi mema kwa ajili ya ujenzi
na ustawi wa maendeleo ya wananchi wa Nigeria; kwa kusimama kidete katika misingi
ya haki na usawa hasa wakati huu Nigeria inapoendelea kuogelea katika mashambulizi
ya kigaidi na ukosefu wa amani na usalama kwa watu wasiokuwa na hatia!
Askofu
mkuu Martins anakichangamotisha Kikundi cha Boko Haram kuheshimu Mfungo wa Mwezi Mtukufu
wa Ramadhani kwa kuachana na vitendo na mashambulizi ya kigaidi.