2014-06-28 15:49:54

Umuhimu wa mchakato wa upatanisho na utulivu wa kisiasa!


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi asubuhi, tarehe 28 Juni 2014 amekutana na kuzungumza na Rais Hery Martial Rajaonarimampianina wa Jamhuri ya Watu wa Madagascar pamoja na ujumbe wake, ambaye baadaye amekutana na kuzungumza pamoja na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Monsinyo Antoine Camilleri, katibu mkuu msaidizi wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Viongozi hawa wawili wamepongeza uhusiano mwema uliopo kati ya pande hizi mbili na wamekazia kwa namna ya pekee mabadiliko yanayoendelea kufanyika nchini Madagascar, pamoja na kuangalia mchango wa Kanisa katika mchakato wa upatanisho wa kitaifa na utulivu wa kisiasa. Wamelipongeza Kanisa kwa kuchangia katika maendeleo ya sekta ya elimu na afya.

Baadaye, Baba Mtakatifu na mgeni wake wamejadili masuala mbali mbali hasa kuhusiana na mapambano dhidi ya baa la umaskini na ukosefu wa usawa kijamii. Wamegusia pia hali ya kimataifa hasa kutokana na kinzani za kivita na kijamii zinazoendelea kugusa maisha ya watu.







All the contents on this site are copyrighted ©.