2014-06-26 11:38:54

Ujumbe wa Kanisa la Kiorthodox kushiriki katika Siku kuu ya Watakatifu Petro na Paulo miamba wa imani!


Katika Mapokeo ya maadhimisho ya Siku kuu ya Mtakatifu Petro na Paulo miamba wa imani, ujumbe wa kiekumene kutoka Kanisa la Kiorthodox kwa mwaka huu 2014 utaongozwa na Askofu mkuu Ioaniss Zizioulas, Makamu wa Rais Tume ya Pamoja ya Kimataifa ya Majadiliano ya Kitaalimungu kuhusu Uekemene.

Tarehe 28 Juni 2014, ujumbe huu wa kiekumene utakutana na kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko na baadaye watazungumza pia na viongozi waandamizi wa Baraza la Kipapa la Uhamasishaji wa Umoja wa Wakristo. Jumapili asubuhi, wajumbe hawa watashiriki katika Ibada ya Misa Takatifu inayotarajiwa kuongozwa na Baba Mtakatifu Francisko kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.

Itakumbukwa kwamba, kila mwaka ifikapo tarehe 30 Novemba wakati wa maadhimisho ya Sherehe ya Mtakatifu Andrea, Baba Mtakatifu hutuma ujumbe wa Kanisa Katoliki kushiriki katika sherehe hizi huko Instanbull, kama mwendelezo wa majadiliano ya kiekumene miongoni mwa Wakristo.







All the contents on this site are copyrighted ©.