Kutokana na kiwango kilichofikiwa cha Tabia Nchi hivi sasa, nchi za Afrika hazina
budi kuungana na kuchukua hatua za kupunguza madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa
kwa pamoja. Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo tarehe 25 Juni, 2014 Mjini Malabo,
Equatorial Guinea wakati akifungua Mkutano wa Wakuu wa Nchi 11 zinazounda Kamati ya
Mazingira ya Nchi za Umoja wa Afrika.
"Suala la Tabia Nchi baranil Afrika
ni changamoto na fursa pia kwani kama tukifanya uamuzi mzuri tunaweza kupata manufaa
kutokana na mbinu mbalimbali zilizopo za kupunguza madhara yake".
Rais
Kikwete amesema na kuzitaka nchi kulichukulia suala la Tabia Nchi kwa umakini mkubwa
kwani kwa hali tuliyofikia hivi sasa, hakuna chaguo lingine bali kuangalia njia za
kupunguza athari zake tu. Nchi wanachama wa Kamati ya Mazingira ya AU in Tanzania
ambaye ndiye Mwenyekiti, Algeria, Ethiopia, Congo-Brazaville, Kenya, Mauritania, Mauritius,
Msumbiji na Uganda.
Kamati ya Mazingira ya AU ina jukumu la kuongoza nchi
za Afrika katika kupanga mikakati, mbinu na njia mbalimbali za kukabiliana na madhara
ya Tabia Nchi barani Agrola na pia kuzitumia changamoto zake katika kuleta maendeleo
na matokeo chanya katika jitihada hizo kwa manufaa ya nchi za Afrika.
Kamati
ya AU imesisistiza kuwa nchi za Afrika zinahitaji kuboresha uwezo wake wa kupata taarifa
za tahadhari katika ngazi zote, uwezo wa kifedha, mawasiliano na usafirishaji katika
miji yake na pia kuongeza uwezo wake wa kuzuia mafuriko kwa kutumia njia za kisasa,
uwezo wa kupanga miji na kupunguza athari za sasa na baadaye kwa ajili ya wananchi
wake na uchumi pia. Amesema pia bara la Afrika linahitaji elimu na maarifa zaidi kwa
wananchi wake kwa ujumla kuhusu athari hizi na tahadhari kwa ujumla.
Rais
amesema pamoja na kwamba nchi za Afrika zinachangia asilimia ndogo katika suala la
Tabia Nchi, Afrika haina budi kuzitaka nchi zinazoendelea kuchangia zaidi katika mahitaji
na juhudi mbalimbali za bara la Afrika katika jitihada zake za kupambana na athari
za Tabia Nchi. Rais Kikwete yuko Malabo kuhudhuria kikao cha siku mbili I cha Wakuu
wa Nchi za Umoja wa Afrika (AU) kinachoanza tarehe 26 Juni 2014 na kumalizika tarehe
27 Juni,2014. Ajenda ya kikao cha Mwaka huu ni Kilimo na Usalama wa Chakula Barani
Afrika.