Hati ya kutendea kazi kwa ajili ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa familia imezinduliwa
mjini Vatican kwa kuongozwa na kauli mbiu "Changamoto za kichungaji kwa familia mintarafu
Uinjilishaji Mpya". Sehemu ya kwanza inawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi
mema kutangaza Injili ya Familia kwa watu wa nyakati hizi.
Sehemu ya pili
ya hati hii inawataka waamini kuangalia mikakati ya shughuli za kichungaji kama njia
ya kupambana na changamoto mpya katika familia. Sehemu ya tatu ni mwaliko kwa Familia
ya Mungu kuwa wazi katika kupokea zawadi ya maisha na kuwajibika katika malezi.
Baba
Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema
kwamba, familia ni kito cha thamani kwa maendeleo ya mwanadamu na jamii katika ujumla
wake!