Wataalam katika sekta ya afya wanasema kwamba, ugonjwa wa Ebola unaendelea kupukutisha
maisha ya watu wengi Afrika Magharibi, kiasi kwamba, kwa sasa kunahitajika rasilimali
watu na fedha ili kukabiliana na mlipiko wa ugonjwa huu. Kwa mara ya kwanza ugonjwa
wa Ebola umejitokeza huko Afrika ya Magharibi hasa nchini Guinea, Sierra Leone na
Liberia.
Ugonjwa huu unaendelea kuenea zaidi kutokana na wananchi wengi kutozingatia
mashariki yaliyowekwa. Watu wanashiriki mazishi hata kwa watu waliofariki dunia kwa
ugonjwa wa Ebola jambo ambalo ni hatari na limeendea kuwa ni chanzo cha kuenea kwa
ugonjwa huu huko Afrika Magharibi. Zaidi ya watu 500 wamekwisha ambukizwa virusi vya
Ebola na zaidi ya watu 300 tayari wamekwisha fariki dunia. Hapa kuna haja ya kupata
madaktari walioandaliwa ili kusaidia kuwaelimisha na kuwatibu watu wanaopambana na
ugonjwa wa Ebola, lakini pia vinahitajika vifaa tiba na dawa ili kutokomeza ugonjwa
wa Ebola.