Sr. Kapuli auwawa kikatili kwa kupigwa risasi kifuani Dar es Salaam!
Sr. Crescentia Kapuli (52) wa Shirika la Bikira Maria Malkia wa Mitume, Jimbo Katoliki
la Mbeya meuwawa kikatili kwa kupigwa risasi kifuani na watu wanaosadikiwa kuwa ni
amajambazi, siku ya Jumatatu alasiri, tarehe 23 Juni 2014 wakati akitoka Benki, eneo
la Ubungo Riverside, Dar es Salaam.
Habari hizi zimethibitishwa na Camillus
Wambura Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kindondoni. Katika tukio hili, Dreva Mark Mwarabu
naye amejeruhiwa kwa risasi na anaendelea kupatiwa matibabu na Polisi inaendelea kufanya
uchunguzi wa tukio hili.
Jimbo kuu la Dar es Salaam Alhamisi tarehe 26 Juni
2014, majira ya saa 5:00 asubuhi linatarajia kuadhimisha Ibada ya Misa takatifu kwenye
Parokia ya Mtakatifu Gaudencia, Makoka kwa ajili ya kumwombea na hatimaye, kuanza
safari kuelekea Jimboni Mbeya, atakapopumzishwa kwenye makao ya milele pamoja na watawa
wenzake.
Marehemu Sr. Crescentia Kapuli alikuwa ni mhasibu wa Shule ya Sekondari
na Chuo cha Ufundi cha Mwenyeheri Anwarite, Makoka na kwamba, mauti yamemfika wakati
akitelekeza utume wake. Kabla ya kuhamishiwa Jimbo kuu la Dar es Saalam, shuleni hapo
aliwahi pia kuwa Mhasibu wa Jimbo Katoliki Mbeya. Familia ya Mungu nchini Tanzania
na kwa namna ya pekee watawa wenzake wameshikwa na simanzi kubwa kuona baadhi ya watu
wenye uchu wa mali wakikaatisha maisha ya Sr. Crescentia Kapuli. RIP.