2014-06-24 14:39:07

Kazi izingatie utu na heshima ya binadamu!


Kanisa linafundisha kwamba, kazi inayo nafasi kubwa katika mchakato wa maboresho ya maisha ya mwanadamu kiroho na kimwili. Watu wanapaswa kuheshimu na kuithamini kazi halali inayowapatia riziki yao ya kila siku. Kazi inajumuisha na kukamilisha hali ya mwanadamu japokuwa kazi sio lengo peke yake katika maisha.

Kwa njia ya kazi mwanadamu anaufanya ulimwengu kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi, kwa kusimamia mafao ya wengi. Mababa wa Kanisa wanasema, utu wa mwanadamu ndicho kipimo cha heshima ya kazi.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema kwamba, anatamani kuwaona watu wengi zaidi wakiwa wanafanya kazi inayoheshimu na kuzingatia utu wa mwanadamu.







All the contents on this site are copyrighted ©.