Rais Danilo Sànchez akutana na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 13 Juni 2014 amekutana na kuzungumza na Rais
Danilo Medina Sànchez kutoka Jamhuri ya Watu wa Domenican ambaye baadaye alikutana
na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu
mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa.
Katika
mazungumzo yao, viongozi hawa wawili wamepongeza uhusiano mwema uliopo kati ya Vatican
na Jamhuri ya watu wa Domenican, lakini zaidi ni kutokana na mchango wa Kanisa Katoliki
nchini humo katika ustawi na maendeleo ya wananchi wote katika sekta ya elimu, afya
na maendeleo endelevu. baba Mtakatifu pamoja na mgeni wake wamegusia pia masuala muhimu
ya kikanda na kimataifa hasa kuhusiano na tatizo la wahamiaji wanaotafuta hifadhi
ya kisiasa bila mafanikio!