(Vatican Radio) Bwana kabla ya kutupa dhamana ya kumtumikia , kwanza hutuandaa ili
tuweze kufanya vizuri. Na mwitikio wetu ni lazim uwe katika misingi ya sala na uaminifu.
Papa amesisitiza katika hotuba yake wakati wa Ibada ya Misa ya asubuhi Ijumaa hii
kaika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta.
Papa alieleza juu ya ujasiri na udhaifu
wa binadamu akisema inaweza kutokea, kwa mpizani jasiri wa ibada ya sanamu katika
huduma ya Mungu, siku moja akasononeka nakukata tamaa hadi kutamani kifo, kwa sababu
tu ya kitisho cha mtu mmoja. Katika majaribu haya, tuna huzunika na poteza matumaini
hata kutamani kufa kwa sababu tu tumepata upinzani, katika kutimiza utume wetu,
mtu mmoja ametutisha. Lakini hakuna sababu za kukata tamaa bali ni kusimama imara
katika utambuzi kwamba, daima ni k azi ya Mungu, kusawazisha hali hizi mbili ujasiri
na udhaifu wa binadamu, siku zote tunapokuwa aminifu kwake. Papa alieleza na kurejea
maelezo juu ya Nabii Eliya kama ilivyoandikwa katika kitabu cha kwanza cha Wafalme.
Katika hotuba yake, Papa Francis alichukua maelezo haya kuwa ni mfano wa uzoefu wa
kila mtu wa imani.
Alisema, wakati Bwana anataka kutupatia ujumbe, anataka
kutupatia kazi, na ni Yeye anayetuandaa sisi kuwa tayari. Anatuandaa kuitenda kazi
yake vizuri kama alivyo mwandaa Eliya. Na jambo la muhimu katika hili si tu kukutana
na Bwana, la hiyo haitoshi. Kilicho muhimu zaidi ni kuishika njia yake na kutembea
humo hadi mwisho wa utume alio tudhaminisha Bwana . Na hii ndiyo tofauti kati ya
kazi za kitume tunazokabidhiwa na Bwana, na kazi zetu za kawaida. Kukamilisha kazi
yake, ni wajibu tena kwa uaminifu na vizuri ... Papa alikamilisha kwa kumeomba
Bwana atupe neema ya kuturuhusu kujiandaa vyema kila siku katika njia ya maisha
yetu, kwa ajili ya kuwa mashahidi wa wokovu wa ulio letwa na Yesu. "