Uje Roho Mtakatifu, uzienee nyoyo za waamini wako. Sala kwa Roho Mtakatifu; Peleka
roho wako vitaumbwa vipya na nchi itageuka.
Tuombe: Ee Mungu, uliyefundisha
nyonyo za waamini ukiwaletea mwanga wa roho mtakatifu, tunaomba tuongozwe na yule
roho, tupende yaliyo mema, tupate daima faraja zake. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo
Bwana wetu amina.
Mhubiri maarufu Padre Raniero Cantalamessa anatoa mfano huu;
bila shaka kila mmoja au wengi wetu tumeshiriki kusukuma au kuona watu wakisukuma
gari bovu. Wengine hukaa nyuma, wengine pembeni n.k isipowaka mara ya kwanza, husimama,
hufuta jasho, hukusanya nguvu tena na halafu hatua ya pili inafuata. Likiwaka, wanaosukuma
hufurahi, hushangilia na hata kupiga miluzi. Maisha yetu ya kikristo huenda hivyo,
pengine kwa nguvu nyingi lakini bila maendeleo thabiti. Leo tunakumbushwa tena na
injili ya kikristo juu ya nguvu kutoka juu inayodai lakini nafasi katika mioyo yetu.
Sherehe ya Pentekoste hutukumbusha tena nafasi ya Roho Mtakatifu katika maisha
yetu na hutupatia tena msukumo mpya wa kiimani.
KATIKA SALA YA NASADIKI: MUNGU
BABA – ANAUMBA MUNGU MWANA AU KRISTO – ANAOKOA MUNGU ROHO MTAKATIFU – ANATAKATIFUZA.
Katika
mwanzo 1; 1-2 tunasoma hivi; hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi, nayo nchi
ilikuwa ukiwa tena utupu na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji. Roho ya
Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
Tunaona kuwa uwepo wa dunia unakuja kwa
tendo la ujio wa Roho ya Mungu. Vile vitu vikapata sura tena ya Mungu. Hivyo Roho
huyo huumba upya na sala tunayosali hapa huwa na maana na sikuku ya leo ina maana
hiyo pia. Je sura yetu kiroho na kimwili ikoje? Dunia yetu ya leo ina sura gani? Maisha
yetu kwa ujumla yana sura gani? Mungu daima anaendelea kuumba - ni ipi nafasi ya Mungu
katika uumbaji wa ulimwengu leo hii?
Ukweli wa kibiblia na zaidi kutoka mwinjili
Yohani - unasema kuwa ufunuo wa Mungu kwetu unawezekana kwa sababu ya ufunuo wa upendo.
Ni Roho Mtakatifu anayetuongoza na kutuwezesha katika ufunuo huo na hii inakuwa wazi
pia katika kumfahamu Kristo na Neno lake. Ni roho atujaliaye hekima na busara ya Kristo
na namna ya kuona. Ni roho inayotuwezesha kuwepo ulimwenguni kadiri ya mapenzi ya
Mungu. Ni huu uwepo wa fumbo, huu muungano na Mungu unaomwezesha mwanadamu kuwepo.
Masomo
yetu ya leo yanatupa mwanga juu ya habari ya Roho Mtakatifu. Lengo la Mtakatifu Luka
kuandika injili na kitabu cha matendo ya mitume ni kuonesha kwa ujumla hali halisi
ya Ukristo.
Pendo la Mungu linalookoa ni kwa kila mmoja, kila mahali na kwa
kila kizazi. Chombo cha utendaji katika kuenenda huko ni Roho Mtakatifu. Mwinjili
Luka anaweka wazi jambo hili - angalia injili ya leo habari juu ya nguvu ya Roho Mtakatifu.
Mtakatifu
Luka anaelewa wazi kuwa huu ndio mwanzo wa kanisa na wajibu wake katika kutangaza
habari njema kwa njia na nguvu ya Roho Mtakatifu.
Katikasomo la kwanza Mtakatifu
Petro anaonesha wazi Roho huyu anatolewa kwa sababu ya kazi ya wokovu ya Yesu Kristo
- Mdo. 2;32-33. Yesu huyo Mungu alimfufua na sisi sote tu mashahdi wake. Basi yeye
akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu na kupokea kwa Baba ile ahadi ya
Roho Mtakatifu amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kusikia. Roho Mtakatifu analeta
pendo la wokovu wa Kristo kwetu sisi. Ndiye Roho huyu tunayepaswa kumpokea na kutenda
naye kazi kama wakristo na katika maisha yetu ya kikristo kila siku. Kinyume chake
ipo hatari ya kuishi roho zetu na si roho wa Mungu aliyetumwa kwetu toka pendo la
Mungu Baba na mwanae Kristo.
Kwetu sisi tunaoamini - tunaweza kuamini na kushuhudia
kwa sababu ya uwepo wa huyo roho. Roho huyo anafanya kazi ndani mwako/yangu/mwetu.
Katikasomo la pili - Mtakatifu Paulo anasema hakuna awezaye kumwita Bwana isipokuwa
katika Roho Mtakatifu. Ukristo wako/wetu ni mpango wa Roho katika kueneza ufalme.
Pentekoste imetokea kwako.
ROHO MTAKATIFU ANA NAFASI GANI KATIKA MAISHA YAKO
AU UNAMWELEWAJE ROHO MTAKATIFU? JE UNATAMBUA UWEPO WAKE? JE WEWE UNAYE ROHO MTAKATIFU
AU UNAISHI MAISHA NA ROHO MTAKATIFU? ROHO MTAKATIFU NI MTENDAJI.
Katika barua
ya Mtume Paulo kwa Wakorintho twaona tabia mbili za kazi ya Roho Mtakatifu. Ugawaji
wa mapaji maalumu kwa waamini na zaidi tukiendelea Paulo anaorodhesha mapaji hayo.
Mengine ni ya pekee kabisa kama kuongea kwa ndimi lakini mengine ni ya kawaida ya
kutekeleza katika maisha yetu ya kikristo ya kila siku kama kufundisha, kusaidia wengine
kwa hali na mali na kuongoza wengine. Muhimu hapa kila tufanyacho tukisaidiana katika
kweli na haki huonesha nguvu ya Roho Mtakatifu ikifanya kazi ndani yetu ni zawadi
yake. Na namna ya kutambua kuwa kama tumepokea zawadi hii au tunaishi zawadi hii ni
kama tu inawasaidia wengine au kama asemavyo mtume Paulo kwa ajili ya faidi ya wote.
Zawadi za Roho Mtakatifu ni kwa wale wote waaminio. Ndo maana mtume Paulo anasema
kuwa zawadi kubwa kabisa ya huyo roho ni UPENDO.
Tabia
ya pili ya Roho Mtakatifu ni nguvu ya kuunganisha. Roho huyo huumba upya katika roho
moja. Sote tumebatizwa katika mwili mmoja. Wakati kila mkristo amepewa karama yake
na roho huyo wote tumekuwa mwili mmoja katika Kristo. Roho Mtakatifu anatuunganisha
sote.
a. Roho Mtakatifu
huonekanaje? Gal. 5: 18-23 – mkiongozwa na Roho hamkai chini ya sheria. Matendo ya
mwili yanatambulikana wazi; ndiyo haya; uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu,
ucheza mazingaombwe, uadui, ugomvi, kijicho, hasira, ubinafsi, utengano, mafarakano,
wivu, ulevi, ulafi na mengineyo kama hayo. …. Lakini matokeo ya Roho ni upendo, furaha,
amani, uvumilivu, hisani, ukarimu, upole, kiasi. Hakuna sheria inayopinga hayo.
b.
Kwa namna ya pekee pia injili ya leo yaunganisha uwepo wa Roho Mtakatifu wa msamaha
dhambi. Roho Mtakatifu anahusishwa moja kwa moja na msamaha wa dhambi. Mitume wanapewa
uwezo wa kusamehe dhambi. Lakini pia kwa namna ya pekee kila wakati ambapo sisi tunasameheana
kati yetu tunatenda hilo kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Hii ni faida kubwa ya ujio wa
Roho Mtakatifu na maana mojawapo ya kufurahi tunapoadhimisha sherehe ya PENTEKOSTE.
c. Ndugu mpendwa imani yako kwa Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu
ni zawadi ya utumishi hata kama ni ndogo kiasi gani. Umoja wako na wengine, uwezo/utayari
wako wa kusema nakusamehe kwa yule aliyekosea yote haya ni alama ya uwepo wa Roho
anayetenda kazi ndani yako. Nenda kafanye hayo/sote tukatende hayo na Roho Mtakatifu
ataonekana kati yetu. Huyo Roho si hewa au maneno mazuri yasiyokuwa na matendo makuu
ya Mungu. Tuishi na kutenda fundisho linavyotuagiza.
Tunaomba. Hekima
- uwezo wa kupambanua kwa njia ya akili mema na mabaya. Kupambanua ukweli na uongo
ili kutoa hukumu kadiri ya sheria ya Mungu.
Hek. 9,1 sala ya kumwomba
Mungu hekima – nakusihi unipe hekima ambayo huketi karibu nawe………….
Katika
Lk 21;15 Yesu anapozungumzia dalili za dhuluma na za ushuhuda anasema kwa sababu mimi
nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala
kuipinga. Akili - kutoa kweli kwa muono wa kina na kupenya kwenye
ukweli wa Mungu.
Shauri
– ili nishike njia nzuri
Nguvu
- kushinda magumu au kuvumilia mateso kwa nguvu na uwezo toka kwa Mungu.
Elimu - kuamua kwa usahihi juu
ya kweli za imani kadiri ya chimbuko halisi na kanuni za kweli zinazofunuliwa.