2014-06-04 10:54:33

Mikakati ya kichungaji kwa ajili ya Zingari


Kanisa na Zingari: Kutangaza Injili pembezoni mwa Jamii, ndiyo tema inayoongoza kongamano la kimataifa kutoka Mabaraza ya Maaskofu Katoliki na Wakurugenzi wa kitaifa kwa ajili ya utume wa Zingari unaonza mjini Vatican kuanzia tarehe 5 hadi 6 Juni 2014 kwa kuandaliwa na Baraza la Kipapa la wahamiaji na watu wasiokuwa na makazi maalum.

Mkutano huu unalenga kufanya upembuzi wa kina kuhusu mikakati ya kichungaji inayotekelezwa na Mama Kanisa kwa ajili ya Zingari, watu ambao hawana makazi maalum na kuangalia ikiwa kama kuna uwezekano wa Kanisa kufanya mabadiliko katika mikakati yake ya shughuli za kichungaji kwa ajili ya Zingari.

Kanisa linajiandaa kufanya kumbu kumbu ya miaka 50 tangu Mtumishi wa Mungu Papa Paulo VI alipotembelea Pomezia na kukutana pamoja na Jamii ya Zingari, huu ukawa ni mwanzo wa mikakati ya kichungaji inayofanywa na Mama Kanisa kwa ajili ya Zingari walionea katika nchi 24 duniani. Ni changamoto ya kufanyia kazi Waraka wa Kichungaji wa Baba Mtakatifu Francisko, Injili ya Furaha "Evangelii gaudium" kwa kuendelea kusoma alama za nyakati.







All the contents on this site are copyrighted ©.