2014-06-03 12:16:12

Asanteni sana walimu!


Kanisa Katoliki limekuwa ni mdau mkuu katika sekta ya elimu kwani elimu ni sehemu ya mchakato wa Uinjilishaji wa kina unaogusa mahitaji ya mtu mzima: kiroho na kimwili.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, anapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru waalimu kwa dhamana na utume wanaotekeleza ndani ya Jamii. Anawakumbusha kwamba, kufundisha ni utume muhimu sana unaowawezesha kuwakaribia vijana ili kuona kilichochema, kizuri na halisi!







All the contents on this site are copyrighted ©.