Vita na utekaji nyara wa watu ni mambo yasiyoweza kuvumilika!
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican anasema, Kanisa limepokea kwa furaha
kubwa kuachiliwa kwa Wamissionari watatu waliokuwa wametekwa nyara tangu mwanzoni
mwa Mwezi Aprili na kuachiliwa huru hapo tare 1 Juni 2014. Baba Mtakatifu Francisko
aliyekuwa anafuatilia kwa makini tukio hili amehabarishwa kuhusu kuachiliwa kwa Wamissionari
hawa na kwamba, Kanisa linamshukuru Mungu kwa tukio hili kuhitimishwa kwa hali ya
amani.
Kanisa litaendelea kusali kwa ajili ya kuombea amani na linawataka
waamini na watu wote wenye mapenzi mema kusimama kidete kupinga aina zote za matumizi
ya nguvu, chuki na vita Barani Afrika na katika nchi nyingine duniani. Bado kuna watu
wasiokuwa na hatia wanaendelea kuteseka kutoka na vita pamoja na kinzani za kijamii
jambo ambalo kamwe haliwezi kuvumiliwa!