2014-05-31 14:46:41

Joyce Banda apigwa chini!


Rais Peter Mutharika wa Malawi, Jumamosi tarehe 31 Mei 2014 ameapishwa kuwa Rais wa Malawi baada ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi nchini Malawi dhidi ya Joyce Banda aliyekuwa Rais wa Malawi, siku chache zilizopita! Peter Mutharika kabla ya kuapishwa kuwa Rais wa Malawi alikuwa ni waziri wa mambo ya nchi za nje wa Malawi na kaka yake Rais Bingu wa Mutharika aliyefariki dunia kunako mwaka 2012.

Katika hotuba yake ya kwanza kama Rais wa Malawi, Bwana Peter Mutharika amewataka viongozi wote waliokuwa kwenye kinyang'anyiro cha kugombea Urais nchini Malawi, kuunganisha nguvu zao kwa ajili ya umoja na mshikamano wa kitaifa. Rais Joyce Banda amekiri kushindwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 20 Mei 2014. Amempongeza Rais Peter Mutharika kwa ushindi wake wa "cheee" na kuwataka wananchi wa Malawi kuheshimu maamuzi ya wapiga kura.

Rais Peter Mutharika ameshinda kwa asilimia 36.4% za kura zote zilizopigwa ambazo ni sawa na kura millioni 1.9.







All the contents on this site are copyrighted ©.