2014-05-30 09:10:39

Rais Peres na Rais Abbas kusali pamoja Vatican


Mkuu wa Ofisi ya habari katika Jimbo Takatifu , Padre Federico Lombardi, Alhamis alithibitisha kwamba mchana Jumapili ya June 8 , 2014, Rais Shimon Peres wa Israel na Rais Mahamoud Abbas wa Palestina, wameitikia mwaliko wa Papa Francisko , kushiriki katika mkutano wa sala Vatican, kwa nia ya kuombea amani.

Papa Francisko, alitoa mwaliko huu akiwa katika ziara yake ya kitume katika Nchi Takatifu, baada ya kuogoza sala ya Malkia wa Mbingu, iliyotanguliwa na Ibada ya Misa kaatika Uwanja wa Hori Takatifu mjini Bethlehemu , Jumapili asubuhi Mei 24 2014.
Katika tukio hili Papa Francisko alisema: ninaitolea nyumba yangu ya mjini Vatican kuwa mahali kwa ajili ya mkutano huu wa sala. Alisema, Mahali hapa ambako Yesu, Mwana Mfalme wa amani alizaliwa , ninapenda kuwaalika Rais Mahmoud Abbas, pamoja na Rais Shimon Peres , kuungana nami kutolea maombi pamoja kwa Mungu, kwa ajili ya zawadi ya amani. Kukutana kwetu hautakuwa wakati wa majadiliano au maongezi ya kutafuta majadiliano , lakini ni kutolea sala kwa Mungu. Sisi sote tunapenda kuishi kwa amani . Sisi sote tunataka amani, alisisitiza Papa ukweli huo, kwamba watu wengi wanapenda kujenga amani siku hadi siku kupitia ishara ndogo ndogo na vitendo ; wengi wanateseka, na bado wana subira katika juhudi za kuleta amani .
Papa alieleza hasa akiwalenga viongozi waliowekwa kwa ajili ya huduma kwa watu, kwamba ni wana wajibu wa kuwa vyombo na wajenzi wa amani , na hasa kupitia sadaka za sala. Papa alionyesha kutambua kwamba, Ujenzi wa amani si jambo jepesi , lakini yamezekana. Kuishi bila amani ni adhabu. Papa alitoa pia himizo kwa wote waume na wake wa nchi hizi, na wa dunia nzima , kila mmoja wao , kuombea amani na kuweka mbele ya Mungu matumaini yao ya dhati kwa ajili ya amani.








All the contents on this site are copyrighted ©.