Kati ya shughuli muhimu zilizofanywa na Baba Mtakatifu siku ya Alhamis ni pamoja na
kukutana na Mheshimiwa Plamen Oresharski , Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Bulgaria. Na
pia alikutana na Mosinyori Francesco Follo , Mtazamaji wa kudumu Shirika la Umoja
wa Mataifa kwa ajili ya Elimu , sayansi na Utamaduni UNESCO.
Aidha aliwateua
kuwa Wajumbe katika Shirika la Mafundisho ya imani Sadikifu ya Kanisa Katoliki: Katibu
wa Jimbo la Papa, Kardinali Pietro Parolin; na Askofu Mkuu Stanislaw Gadecki ya Poznan,
Poland, na rais mpya wa Baraza la Maaskofu Poland , Askofu Rudolf Voderholzer na
Askofu wa Regensburg, Ujerumani.