2014-05-30 15:15:11

Maisha ya Mkristo si lelemama siku zote


Ni lazima kusema ukweli : maisha ya Kikristo si lelemama muda wote . Ni vyema kutambua na kukubaliana kwamba, pia kuna wakati wa kulia na kuteseka, wakati wa kuugua , wakati wa matatizo ya kifamilia,ya watoto, ya mke, ya mme na hata matatizo ya kiuchumi , kuona kwamba mshahara hauwezi kukidhi mahitaji ya familia hadi mwisho wa mwezi,licha ya kuwa na mtoto au mke au mme mgonjwa. Pengine hata inakuwa vigumu kulipa kodi ya nyumba au mkopo wa nyumba au matatizo mengine mengi yanayokabili jamii.

Lakini Yesu anatuambia tusiwe na hofu. Tusiwe watu wa huzuni , au watu wa kulilia tu na kuhuzunika, ila tuwe watu wa kufurahi tu hata katika matatizo na hata wakati watu wanapotuudhi au kutochokoza. Ni mahubiri ya Papa Francisko, mapema siku hii ya Ijumaa,wakati akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la mjini Vatican.

Papa alikiri kwamba wakati wa matatizo mara nyingi tunalisahau ahadi hii ya Yesu kwmba, tusiogope. Tunasahau kwamba, mateso ni wakati wa kuwa na furaha kwa sababu ni wakati wa kujitakasa kwa shuhuida za maisha ya kila siku. "Huzuni yako inarejea kuwa furaha, ingawa ni vigumu kufurahia wakati unateseka kwa maradhi au kuw ana mtoto mgonjwa". Lakini Yesu anasema, "jipeni moyo! Haya! Kesho utakuwa na furaha".

Papa alihimiza, yatupasa kusikiliza wito huu wa Yesu , unaotuondoa katika giza, wakati ambao hatuoni matumaini yoyote. Na Papa alionyesha imani yake kwa Bwana kwamba, Bwana anao uwezo wote wa kuigeuza huzuni hii na kuwa furaha . Na kwamba hajui kwa jinsi gani, lakini anajua ni hivyo. Ni kupitia kitendo cha imani katika Bwana. Tendo la imani !

Daima kuwa jasiri katika mateso na kufikiri kwamba baadaye, Bwana anakuja kwa furaha kufuta giza hili la mateso . Bwana aliachia ahadi hii, na sisi sote tunapaswa kuyapokea yote katika furaha hii, ya matumaini. Na ishara kwamba tuna furaha hii kwa matumaini ya amani . Wangapi wagonjwa, ambao mwishoni mwa maisha na maumivu, wao sasa wamepumzika kwa amani kiroho?

Hili linapaswa kuwa mbegu ya furaha yetu , furaha ya tumaini na amani, Papa alieleza na kuhoji iwapo tuna amani kiroho wakati wa giza, wakati wa taabu, wakati wa mateso , wakati mgonjwa wetu, ? Je, tuna amani ? Kama una imani , una mbegu ya furaha kwamba atakuja baadaye. Na alisali ili Bwana atuwezeshe kuelewa mambo haya .








All the contents on this site are copyrighted ©.