Baba Mtakatifu Francisko anaendelea kumwimbia Mwenyezi Mungu utenzi wa sifa na shukrani
kwa kuhitimisha hija ya kitume iliyomwezesha kusherehekea Jubilee ya Miaka 50 tangu
Papa Paulo VI alipokutana na kusali na Patriaki Anathegoras; kuwaimarisha wote wanaojibidisha
katika mchakato wa kutafuta amani huko Mashariki ya Kati pamoja na kuwaimarisha ndugu
zake katika imani.
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii anawaalika kujenga urafiki wa dhati na Yesu Kristo, ili waweze
kumfuasa kwa ukaribu zaidi na hatimaye, kuishi pamoja na kwa ajili yake!