Mama Meriam Yahaya Ibrahim Ishaq, aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kuasi dini
ya Kiislam na kuolewa na Mkristo, amejifungua mtoto wake wa pili akiwa gerezani. Mama
Meriam anasema katika maisha yake hajawahi hata siku moja kuwa ni mwamini wa dini
ya Kiislam, lakini kadiri ya Sharia, mtoto wa Mwamini wa dini ya Kiislam ni Muislam
tu!