2014-05-26 09:57:30

Maeneo ya Nchi Takatifu- yawezekana kuishi kwa amani-Papa .


Jumapili baada ya Ibada ya Misa, mjini Bethlehemu , Baba Mtakatifu Francisko aliekea Jerusalem , ambako alipokelewa na Rais wa Jamhuri ya Israel, Shimon Peres na Waziri Mkuu , Benjamin Netanyahu , katika uwanja wa ndege wa Ben Gourion wa Tel Aviv Jerusalem.
Katika hotuba ya mapokezi , viongozi hao walionyesha hofu kubwa kwa vurugu zinazoendelea Mashariki ya Kati, ambako mara nyingi Wakristo huteswa. Na kwamba yawezekana kuishi kwa amani katika eneo hilo lenye urithi mkubwa wa historia ya dini kuu tatu. Wayahudi, Wakristu na Waislamu .
Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu , katika hotuba yake ya kumkaribisha Papa aliitaja, Israel kwamba imekuwa “kisiwa” cha uvumilivu katika kuhakikisha haki kwa wote. Na kwamba wanapania kutetea haki za watu wote, wanaoishi Maeneo Mtakatifu, licha ya tofauti za imani zao.

Na Papa Francisko , katika hotuba yake , alitoa shukurani zake kwa moyo wa ukarimu na mapokezi mazuri waliyompatia mara baada ya kuingia nchini Israel. Na kwamba kwake ilikuwa ni furaha kuu kufanya hija katika nchi Takatifu akifuata nyayo za watangulizi wake, ambayo ina historia ya miaka 50 iliyopita, iliyofanywa na na Papa Paulo V1.

Papa alikiri tangu wakati ule hadi sasa , kuna mabadiliko mengi yaliyofanyika kati ya Jimbo Takatifu na Nchi ya Israel, katika mahusiano ya Kidiplomasia , ambayo kwa sasa yanafikisha miaka ishirini ya uwepo wake. Mahusiano yanayo endelea kufanikisha mwendelezo wa mahusiano mazuri na urafiki , kama ilivyoshuhudiwa katika uwekaji wa sahihi katika makubaliano na mikataba na njia ya kutembea pamoja katika kufanya marekebisho ya hapa na pale. Kwa roho hiyo ya mshikamano na umoja Papa alitoa salaam zake za kipapa kwa watu wote wa Israel na kuwatakia kila la heri, amani na ustawi wa kiroho na kihali pia.
Hotuba ya Papa, ilikumbusha msisitizo uliokwisha tolewa na watangulizi wake, katika kudumisha historia na misingi ya urithi wa kuzaliwa kwa dini kuu tatu katika eneo hilo, Wayahudi, Wakristu na Waislamu. Dini ambazo zote, msingi wake wa imani kiroho , umesimiskwa katika kujali ubinadamu. Na hivyo Papa Fransiciko alionyesha tumaini lake kwamba katika nchi hii Takatifu , hapatakuwa na nafasi , kwa wale wanao taka kutumia dini kama chombo cha kuchochea kutovumiliana , ghasia na maonevu kwa yoyote yule.
Papa aliendelea kutaja kama hitaji la dharura, kufanikisha amani si tu kwa Israel lakini katika mkoa wote wa Nchi Takatifu. Papa aliasa dhidi ya ongezeko la ghasia na uchokozi unaofanyika mara kwa mara na kuvuruga imani na kusababisha mateso makubwa kwa watu .

Akiwa ameshimana katika umoja na watu wote wenye mapenzi mema, Papa aliwataka wote wale wenye kuwa na mamlaka , kuwajibika kikamilifu katika juhudi za upatikanaji wa majawabu thabiti, ikiwemo ufutaji matatizo mazito yaliyopo kati ya Israel na Palestina , ili wote waweze kuishi kwa amani na mapatano.
Kwa upande wa Kanisa, kati ya walifika kumlaki Papa katika uwanja huu wa Tel Aviv, ni pamoja na Nunsio wa Mjumbe wa Kitume wa Papa nchini Israel, Askofu Mkuu Giuseppe Lazzarotto.









All the contents on this site are copyrighted ©.