2014-05-26 12:32:36

Azimio la Pamoja la Papa Francisko na Patriaki Bartholomeo I


Baba Mtakatifu Jumapili akiendelea na ziara yake, pia alikutana katika hali ya faragha na Patriaki Barthlomew I, wa Kiekumene wa Costantinople , ukiwepo pia ujumbe wa kitume wa Jerusalem na Katibu wa Vatican , Kardinali Pietro Parolin, na Mkuu a Shirika kwa ajili ya Umoja wa Wakristu, Kardinali Kurt Koch
Baada ya mkutano wao, kulitolewa azimio la pamoja, la Papa Francisko na Partriaki Bartholomew 1, ambamo wametoa heshima zao kwa watangulizi wao , Papa Paul VI na Patriaki wa Kiekumeni Athenagoras , ambao walikuwa na ujasiri wa kukutana Yerusalemu miaka hamsini iliyopita. Na hivyo wao pia , Papa Francisko na Patriaki Bartholomayo I , wamefanya mkutano wao katika eneo hili la Nchi Takatifu, "ambapo mkombozi wetu Kristo Bwana, aliishi, kufundisha, alikufa , akafufuka na akapaa mbinguni , ambapo yeye alimtuma Roho Mtakatifu juu ya changa Kanisa kama pia maelezo yalivyo tolewa Papa Paulo VI na Patriaki Athenagoras , yaliyo chapishwa baada ya mkutano wao , Januari 6, 1964.

Na pia wametaja Mkutano wao wa ziada wa Maaskofu mjini Roma na Constantinople , katika mtiririko wa udugu wa mitume wawili, Petro na Andrea, chanzo cha furaha na uthabiti wa kiroho, wenye kuwapa nafasi ya kutafakari kina na uhalisi wa uhusiano kati yao , na matokeo ya safari ndefu ya kuwa wamoja, iliyojaa neema hiyo ambayo Bwana, aliimimina kwao, tangu siku hiyo heri ya miaka hamsini iliyopita .

Azimio limeendelea kutaja kukutana kwao kindugu , kuwa ni hatua nyingine mpya na muhimu katika njia ya kuelekea umoja ambayo Roho Mtakatifu pekee ndiye anaweza kuwaongoza katika ushirika wenye kuwa na utofauti halali. Tunakumbuka kwa shukrani hatua ambazo Bwana tayari ametupa kukamilisha.

3. Na kwa kufahamu kwamba, umoja huu, wazi ni upendo wa Mungu na upendo kwa jirani , wao kwa muda mrefu, siku hadi siku, hatimaye wameweza kushiriki pamoja katika karamu ya Ekaristi. Na kama Wakristo, wana wajibu wa kujiandaa kupokea zawadi hii ya Ushirika Mtakatifu , kama alivyofundisha Mtakatifu Irenaeus wa Lyons , kwa njia ya ungamo la imani na sala za pamoja za mara kwa mara,na kubadilika muono wa ndani, upya wa maisha na mazungumzo ya kidugu (taz. Yn 13:35).

4. Kwa maana hii, majadiliano muhimu kwa ajili ya kutafuta ushirika kamili kati ya Wakatoliki na Wa-Orthodosi, yataendelea kama ilivyo katika majadiliano ya kitheolojia yanayo fanywa na Tume ya Kimataifa ya Pamoja .

5.Wakiwa bado katika njia ya kuelekea ushirika kamili , wao wana wajibu wa kutoa ushahidi katika kila hali za kawaida, kuonesha upendo wa Mungu kwa ajili ya wote na kufanya kazi pamoja kwa ajili ya huduma kwa ubinadamu , hasa kuhusiana na ulinzi wa hadhi ya binadamu katika kila hatua ya maisha na heshima ya familia ya msingi juu ya ndoa , kukuza amani na manufaa ya wote, kama jibu kwa taabu na mahangaiko yanayoendelea kuwa mapigo katika dunia yetu. Tunatambua kwamba ni lazima daima, kuwa mstari wa mbele kusaidia watu wahitaji zaidi hasa wanaokabiliwa na njaa, umaskini , ujinga, na usambazaji usiokuwa wa usawa wa bidhaa. Ni wajibu wetu kujitahidi pamoja ili kujenga tu na ubinadamu jamii ambayo hakuna mtu kutengwa au kubaguliwa.

6.Na kwa undani wanaamini kwamba, hali ya baadaye ya familia ya binadamu inategemea sana kizazi cha sasa, na wao kama viongozi. Na hivyo baada ya kupima kwa busara na upendo, na haki na usawa , na zawadi ya uongozi waliokabidhiwa na Mungu na kisha kutubu, kutambua ugandamizaji haki unaoendelea duniani sasa, , ambayo ni dhambi mbele ya Mungu, vinawathibitishia wajibu wao katika kulea hisia ya unyenyekevu na kiasi , ili wote wapate hisi ya haja ya kuheshimu viumbe na kulinda mazingira kwa uangalifu. Na hivyo kwa Pamoja , wamethibitisha wajibu wao wa kuamsha dhamiri kuelekea ulinzi wa uumbaji , kwa kutoa Tunatoa wito, kwa wanaume na wanawake wote wenye mapenzi mema kuangalia, njia yao ya maisha, kwa moyo wa kiasi zaidi ,na kuzimisha moyo wa uchoyo na kuinua zaidi ukarimu, kwa ajili ya ulinzi wa ulimwengu wa Mungu na kwa manufaa ya watu wake.

7. Pia kuna haja ya haraka kwa ajili ya ushirikiano thabiti na kutimiza ahadi miongoni mwa Wakristo, ili kulinda kila mahali haki ya kutoa hadharani imani yao na kutendewa haki wanapo timiza nia ya kukuza mchango kwamba Ukristo ni sehemu ya maisha kwa jamii na hata katika utamaduni wa kisasa . Katika suala hili , tunawaomba Wakristo wote kukuza mjadala wa kweli na Wayahudi, na Uislamu na mila nyingine za kidini. Kutofautiana na utoaji wa majibu bila ufahamu, huweza tu kusababisha kukosa uaminifu na kwa bahati mbaya, hata migogoro.

8. Kutokana na hili, wakiwa katika Mji Mtakatifu wa Yerusalemu , walipenda kueleza wasiwasi wao, kwa hali ya kawaida ya Wakristo katika Mashariki ya Kati na kwa haki yao ya kuwa raia kamili ya nchi zao .Na kwa ujasiri walitolewa maombi yao kwa Mwenyezi Mungu mwenye huruma kwa ajili ya amani katika Nchi Takatifu na Mashariki ya Kati . Wanaomba hasa kwa ajili ya makanisa nchini Misri , Syria na Iraq, ambako yanakumbana na mateso makali, kama iliyokuwa katika matukio ya hivi karibuni . Na hivyo wanahimiza pande zote , bila kujali imani za dini zao , kuendelea kufanya kazi kwa maridhiano na kwa kutambua haki sahihi za watu . Kwa undani wanaamini kwamba silaha si nyenzo ya kujenga amani ya kudumu, bali njia mazungumzo , msamaha na upatanisho ndiyo njia sahihi ya kuifikia amani ya kweli.

Na hivyo wametoa wito kwa Wakristo, waamini wa mila zote za kidini na watu wote wenye mapenzi mema , kutambua kama jambo la dharura , kuushiriki kikamilifu juhudi zote zinazo tafuta maridhiano na umoja wa familia ya kibinadamu , kwa heshima kamili kwa ajili ya tofauti halali kwa ajili ya mema ya binadamu wote na kwa vizazi vijavyo.

Na wakiwa katika Hija hii ya kawaida na mahali ambapo Bwana wetu pekee, Yesu Kristo alisulubiwa , akazikwa na kufufuka tena , kwa unyenyekevu, wanajikabidhi katika maombezi ya Mama Bikira Maria, katika kupata ujasiri wa kutembea pamoja katika safari hii ya kuelekea umoja kamili, katika Upendo wa Mungu usiokuwa na mwisho kwa ajili ya familia nzima ya binadamu.

"Bwana na akuangazie uso wake na huruma yake . . Bwana akuonyeshe uso wake na kukupa amani "( Nm 6, 25-26).








All the contents on this site are copyrighted ©.