2014-05-25 10:41:12

Jacob Zuma, mtemi Afrika ya Kusini!


Rais Jacob Zuma aliyeshinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni nchini Afrika ya Kusini, Jumamosi tarehe 24 Mei 2014 ameapishwa rasmi na kuanza kuwaongoza wananchi wa Afrika ya Kusini katika awamu ya pili ya uongozi wa Serikali yake.

Tukio hili limeandamwa na maandamano ya kumpinga Rais Zuma kwamba ni kiongozi ambaye hastahili kuwaongoza wananchi wa Afrika ya Kusini kutokana na kashfa ya ufisadi wa mali ya umma inayomwandama, kwa kutumia kiasi cha dolla za kimarekani millioni 23 kwa ajili ya ukarabati wa nyumba yake binafsi.

Rais Zuma anashutumiwa pia kwa kuitumbukiza Afrika ya Kusini katika hali mbaya ya uchumi. Pamoja na mambo yote haya wachunguzi wa mambo wanasema, demokrasia imeshika mkondo wake na wananchi wa Afrika ya Kusini wamemchagua Rais Zuma kuwaongoza tena kwa awamu ya pili! Tukio hili limehudhuriwa na viongozi mbali mbali kutoka Afrika!







All the contents on this site are copyrighted ©.