2014-05-24 09:10:01

Ukatili dhidi ya ubinadamu!


Kamati ya Mkataba Dhidi ya Ukatil ya Umoja wa Mataifa, CAT imehitimisha kazi ya kupembua taarifa ya utekelezaji wa itifaki hii kutoka Vatican na kuipongeza kutokana na mabadiliko makubwa yaliyofanywa na Vatican katika kukabiliana na na ukatili na mambo yote yanayodhalilisha utu na heshima ya binadamu. Kamati hii imefurahishwa kwa namna ya pekee na majadiliano katika ukweli na uwazi yaliyooneshwa na ujumbe wa Vatican kwenye mkutano huu.

CAT INASEMA haijatamka kwamba, Vatican na wadau wake mbali mbali hawajavunja mkataba wa CAT. Kamati hii inatambua juhudi zilizofanywa na Kanisa, Majimbo na Mashirika ya kitawa katika mchakato wa kudhibiti nyanyaso za kijinsia dhidi ya watoto wadogo Kanisa na taasisi zake zimewasaidia wahanga wa nyanyaso za kijinsia kwa kuwalipa fidia kiasi cha dolla za kimarekani billioni 2.5 tangu mwaka 1950 na kwamba, kiasi cha dolla za kimarekani millioni 78 kimetengwa kwa ajili ya matibabu na huduma nyingine.

CAT imekataa ushauri wa ujumbe wa Vatican kutafsiri na kuhusisha suala la utoaji mimba kama unyama na ukatili dhidi ya binadamu, ili kulinda uhuru wa kidini na maoni kuhusu kulinda na kudumisha maisha ya binadamu. CAT pia imekataa kuhusisha vitendo vya kubaka na nyanyaso za kijinsia kuhusishwa katika adhabu zinazotolewa na kamati. Ujumbe wa Vatican umepokea ushauri ambao utafanyiwa kazi kwa wakati muafaka katika utekelezaji wa Mkataba dhidi ya ukatili wa binadamu.

Akifafanua kuhusu taarifa ya CAT, Askofu mkuu Silvano Maria Tomasi anasema kwamba, Vatican ilijiunga na itifaki ya mkataba huu kunako mwaka 2002. Mkutano uliochambua taarifa ya awali kutoka Vatican, ulifanyika kati ya tehe 5 hadi 6 Mei, 2014. Ifahamike kwamba, Mapadre, kisheria wako chini ya Maaskofu wao mahalia na kwamba, Kanisa linaendelea kujielekeza zaidi na zaidi katika kulinda na kutetea utu na heshima ya binadamu kama inavyoonekana katika maisha na utume wa Baba Mtakatifu Francisko.

Kanisa bado linaendelea kukazia toba na wongofu wa ndani pamoja na majiundo makini ili kuepuka kashfa za nyanyaso za kijinsia zilizolikumba Kanisa katika miaka ya hivi karibuni. Kanisa litaendelea kujielekeza zaidi katika huduma za kichungaji na uinjilishaji mpya kama kielelezo cha uaminifu kwa Kristo na Kanisa lake!







All the contents on this site are copyrighted ©.