Baba Mtakatifu Francisko tarehe 30 Mei 2014 majira ya jioni anatarajiwa kumweka wakfu
Monsinyo Fabio Fabene, Katibu mkuu msaidizi wa Sinodi za Maaskofu kuwa Askofu, ili
kuimarisha mchakato wa utekelezaji wa maadhimisho ya Sinodi kama chombo muhimu sana
katika maisha na utume wa Kanisa.
Itakumbukwa kwamba, Askofu mteule Fabio
Fabene alizaliwa mjini Roma, tarehe 12 Machi 1959. Baada ya masomo na majiundo yake
ya kikasisi, akapadrishwa tarehe 26 Mei 1984. Baba Mtakatifu Francisko akamteuwa kuwa
Askofu hapo tarehe 8 Aprili 2014.